• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

Jamii yasisitizwa kuendelea kuchukua tahadhari

Posted on: March 3rd, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi ameonyesha kuridhishwa kwake na utendaji kazi wa kitengo kinachosimamia utekelezaji wa afua mbalimbali katika kitengo cha magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kwa namna ambavyo kimekuwa kikifanya majukumu yake na kutoa mrejesho chanya katika utekelezaji wake kwani kimekuwa chachu ya mabadiliko katika jamii ambapo kwa zaidi ya asilimia 75 matokeo ya utekelezaji ni mazuri huku akitaka na vitengo vingine vilivyoko chini ya idara ya afya kuongeza juhudi ili kuwa na mabadiliko chanya kwenye jamii.

Akitoa pongezi hizo Machi 3 mwaka huu Mgoyi amesisitiza jamii kiujumla kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa corona kwa kuzingatia maelekezo yote yanayotolewa na wataalam wa afya kwani misiba katikati ya jamii imekuwa mingi hivyo ni vema jamii ikaendelea kupata elimu na kuchukua tahadhari ikiwemo kuvaa barakoa na tahadhari nyinginezo.

Aidha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Asajile Mwambambale amewataka viongozi wote wa vitengo mbalimbali vilivyoko katika idara kuwajibika kwa sehemu yao na kufanya kazi zenye kuleta tija badala kumwachia majukumu yake mkuu wa Idara au Mkurugenzi au Mkuu wa Wilaya kwani kila mtu anao wajibu wa kuwajibika na kujitoa kwa dhati kufanya kazi katika eneo lake kikamilifu kwa lengo la kuleta matokeo chanya.

Pamoja na hayo amesema Halmashauri imejipanga kwa dhati kufanya mabadiliko makubwa katika sekta mbalimbali hususani sekta ya afya ambapo suala la lishe litapewa kipaumbele kwa umuhimu wake ili kuwa na jamii yenye afya bora huku akikitaka kitengo kinachoshughulika na suala la utoaji dawa mashuleni kwa ajili ya wanafunzi kutoa ratiba mapema ili idara zinazohusika ziweze kuweka taratibu zinazostahiki ikiwemo upatikanaji wa chakula mashuleni.

Naye Mratibu wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Wilaya Rosemary Nguruwe  amesema kuwa kwa asilimia kubwa shughuli zilizopangwa zimefanyika huku akisema kuwa zaidi ya asilimia 95 ya fedha zimetumika kama ilivyopangwa, lakini pia ushirikiano mzuri kati ya miradi mingine ,kuongezeka kwa wanafunzi wanaomeza dawa kila mwaka pamoja na ushiriki mzuri wa wadau mbalimbali katika shughuli za NTDs wakiwemo viongozi wa dini na Chama Tawala (CCM) huku baadhi ya changamoto zilizojitokeza ni shule nyingi kutokuwa na chakula, ushiriki mdogo wa viongozi hasa katika vitongoji, utoaji wa  fedha kuchukua muda mrefu, kutofanyika kwa zoezi kwenye jamii mwaka 2020 na mawasiliano hafifu kwa baadhi ya ofisi.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa