• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mipango
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mifungo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

Jamii yasisitizwa kuendelea kuchukua tahadhari

Posted on: March 3rd, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi ameonyesha kuridhishwa kwake na utendaji kazi wa kitengo kinachosimamia utekelezaji wa afua mbalimbali katika kitengo cha magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kwa namna ambavyo kimekuwa kikifanya majukumu yake na kutoa mrejesho chanya katika utekelezaji wake kwani kimekuwa chachu ya mabadiliko katika jamii ambapo kwa zaidi ya asilimia 75 matokeo ya utekelezaji ni mazuri huku akitaka na vitengo vingine vilivyoko chini ya idara ya afya kuongeza juhudi ili kuwa na mabadiliko chanya kwenye jamii.

Akitoa pongezi hizo Machi 3 mwaka huu Mgoyi amesisitiza jamii kiujumla kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa corona kwa kuzingatia maelekezo yote yanayotolewa na wataalam wa afya kwani misiba katikati ya jamii imekuwa mingi hivyo ni vema jamii ikaendelea kupata elimu na kuchukua tahadhari ikiwemo kuvaa barakoa na tahadhari nyinginezo.

Aidha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Asajile Mwambambale amewataka viongozi wote wa vitengo mbalimbali vilivyoko katika idara kuwajibika kwa sehemu yao na kufanya kazi zenye kuleta tija badala kumwachia majukumu yake mkuu wa Idara au Mkurugenzi au Mkuu wa Wilaya kwani kila mtu anao wajibu wa kuwajibika na kujitoa kwa dhati kufanya kazi katika eneo lake kikamilifu kwa lengo la kuleta matokeo chanya.

Pamoja na hayo amesema Halmashauri imejipanga kwa dhati kufanya mabadiliko makubwa katika sekta mbalimbali hususani sekta ya afya ambapo suala la lishe litapewa kipaumbele kwa umuhimu wake ili kuwa na jamii yenye afya bora huku akikitaka kitengo kinachoshughulika na suala la utoaji dawa mashuleni kwa ajili ya wanafunzi kutoa ratiba mapema ili idara zinazohusika ziweze kuweka taratibu zinazostahiki ikiwemo upatikanaji wa chakula mashuleni.

Naye Mratibu wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Wilaya Rosemary Nguruwe  amesema kuwa kwa asilimia kubwa shughuli zilizopangwa zimefanyika huku akisema kuwa zaidi ya asilimia 95 ya fedha zimetumika kama ilivyopangwa, lakini pia ushirikiano mzuri kati ya miradi mingine ,kuongezeka kwa wanafunzi wanaomeza dawa kila mwaka pamoja na ushiriki mzuri wa wadau mbalimbali katika shughuli za NTDs wakiwemo viongozi wa dini na Chama Tawala (CCM) huku baadhi ya changamoto zilizojitokeza ni shule nyingi kutokuwa na chakula, ushiriki mdogo wa viongozi hasa katika vitongoji, utoaji wa  fedha kuchukua muda mrefu, kutofanyika kwa zoezi kwenye jamii mwaka 2020 na mawasiliano hafifu kwa baadhi ya ofisi.

Tangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI October 11, 2021
  • ZABUNI January 31, 2017
  • SOMA KATIBA ILIYOPENDEKEZWA March 24, 2017
  • UTARATIBU WA UHAMISHO KWA WATUMISHI WA UMMA March 24, 2017
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • Kilosa kufanya sensa ya mifugo

    December 29, 2022
  • Kilosa kunufaika na mradi wa BOOST

    December 24, 2022
  • Kilosa yaendelea kutambua juhudi za Serikali kwa Watumishi wa Umma na Wananchi-DED Kilosa

    December 19, 2022
  • -Serikali haitosita kulinda Rasilimali watu kwa maslahi ya Maendeleo ya Taifa- Mh. Mhagama

    December 20, 2022
  • Angalia zote

Video

HIFADHII YA WANYAMA MIKUMI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • MFUMO WA PLANREP

Kurasa za Mfanano

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • NECTA
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737-847-880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa