• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mipango
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mifungo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

JENGENI ARI YA KUJILETEA MAENDELEO

Posted on: May 22nd, 2019

Wito umetolewa kwa wananchi wote kujenga ari na hulka ya kujiletea maendeleo wenyewe kwa kujikita katika shughuli za uzalishaji hasa katika kilimo cha miwa kutokana na uwepo wa mabonde yanayofaa kwa kilimo hicho ikiwemo bonde la ihombwe ambalo linafaa kwa kilimo hicho na kwamba hiyo ni fursa adhimu na yenye tija.

Wito huo umetolewa Mei 21 mwaka huu na Kaimu Afisa Tawala Reginald Simba aliyemwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Kilosa katika sherehe ya wakulima wa miwa wa bonde la Ihombwe , Kitunduweta, Mhenda na Ilakala sambamba na kuweka jiwe la msingi katika ofisi ya kampuni ya Geoman Cane Estate ltd sherehe zilizokwenda kwa kauli mbiu ya wakati ni sasa tajirika na miwa.

Simba amesema kuwa ili kuweza kuufikia uchumi wa kati ni vema kujikita katika shughuli za uzalishaji mali ambapo serikali ya awamu ya tano inahimiza wawekezaji kuwekeza pamoja na kuanzisha viwanda kwani uwepo wa viwanda katika maeneo yetu ni fursa nzuri sana ya ajira kwa watu mbalimbali

Aidha amempongeza mwekezaji Dkt. George Mlingwa kwa jitihada zake za kuwa bega kwa bega na wakulima wa miwa ambapo mwekezaji huyo anatarajia kujenga kiwanda cha sukari katika eneo la Ihombwe jambo linalotokana na ongezeko la uzalishaji miwa ambapo pia katika juhudi za kuleta maendeleo katika jamii kampuni ya Geoman kwa kushirikiana na kijiji cha Ihombwe imefanikisha ujenzi uliokamiliaka wa darasa la chekechea pamoja na kuchimba visima viwili ambapo kimoja tayari kimeanza kutumika na wananchi kwa maji safi na salama.

Akisoma risala yake mbele ya mgeni rasmi Mkurugenzi wa kampuni ya Geoman Dkt George Mlingwa amesema kuwa katika mazao ya biashara yote duniani hakuna zao lenye faida kubwa kama zao la miwa kwani ni zao lenye faida.

Akizungumzia upande wa uanzishaji kiwanda cha sukari Dkt Mlingwa amesema kuwa kutokana na ongezeko la uzalishaji miwa kampuni ya Geoman inatarajia kuanza ujenzi wa kiwanda cha miwa mwaka huu na kukamilika Juni 2020 na kwamba uwepo wa kiwanda hicho utahamasisha sana kilimo cha miwa  na kupelekea tatizo la kupeleka miwa Kilombero kuisha kabisa sambamba na kushuka kwa gharama za usafirishaji ambapo pia miwa hiyo itasagwa ikiwa bado sacrose kubwa.

Sambamba na hayo Dkt Mlingwa amesema kuwa licha ya changamoto ya tatizo la miundombinu duni katika maeneo ya uzalishaji miwa, tatizo la barabara kuu itokayo Kilosa –Mikumi pamoja na upatikanaji wa ardhi ambapo ameomba serikali kuzitupia jicho la karibuchangamoto hizo, kampuni ya Geoman kama mwekezaji imebuni miradi miwili katika kukuza zao la miwa kwa kuwa na mradi wa uwezeshaji unaowezesha wakulima wapya kulimiwa shamba kati ya nusu eka na ekari moja na kupatiwa mbegu ambapo mradi wa pili ni mradi wa ubia ambapo mkulima anaingia ubia na kampuni.

Kutokana na miradi hiyo tunategemea kuwa zao la miwa litalimwa ka kasi kubwa na hadi kufikia 2025 uzalishaji wa mkiwa katika bonde la ihombwe utafikia tani 50,000 za miwa zenye uwezo wa kuzalisha tani 5000 za sukari huku kimapato zinategemewa kupatikana shilingi bilioni tano kwa 2025. Dkt. Mlingwa ameongeza

Tangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI October 11, 2021
  • ZABUNI January 31, 2017
  • SOMA KATIBA ILIYOPENDEKEZWA March 24, 2017
  • UTARATIBU WA UHAMISHO KWA WATUMISHI WA UMMA March 24, 2017
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • Kilosa kufanya sensa ya mifugo

    December 29, 2022
  • Kilosa kunufaika na mradi wa BOOST

    December 24, 2022
  • Kilosa yaendelea kutambua juhudi za Serikali kwa Watumishi wa Umma na Wananchi-DED Kilosa

    December 19, 2022
  • -Serikali haitosita kulinda Rasilimali watu kwa maslahi ya Maendeleo ya Taifa- Mh. Mhagama

    December 20, 2022
  • Angalia zote

Video

HIFADHII YA WANYAMA MIKUMI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • MFUMO WA PLANREP

Kurasa za Mfanano

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • NECTA
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737-847-880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa