• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

Kabudi akabidhi mifuko 200 ya saruji shule ya sekondari Mabula

Posted on: January 31st, 2021

Mbunge wa Jimbo la Kilosa ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof Palamagamba Idan Kabudi amekabidhi saruji mifuko 200 sawa na tani kumi yenye thamani ya kiasi cha shilingi milioni 3.2 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya Sekondari Mabula iliyopo katika kata ya Mabula wilayani Kilosa mkoani Morogoro.

Mbunge wa Jimbo la Kilosa Mkoani Morogoro Prof Palamagamba Kabudi
 akikabidhi Mifuko ya Saruji shule ya Sekondari Mabula.

Akikabidhi mifuko hiyo Januari 30 mwaka huu Kabudi amesema kuwa ameamua kutoa fedha zake binafsi kununua mifuko hiyo lengo likiwa ni kusaidia kufanikisha ujenzi wa vyumba ili wanafunzi waliofaulu na kuchaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu waweze kuanza masomo mapema mara baada ya ujenzi kukamilika .

Mh. Kabudi akiteta jambo na Afisa Mipango Wilaya Francis Kaunda

Aidha amewataka wanafunzi hao kusoma kwa bidiii ili waweze kufanya vizuri katika mitihani yao na kwamba atakuwa mstari wa mbele kuwasaidia katika kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili.

Mwanafunzi Elieza Chibula (katikati) akitoa shukrani zake

 kwa mbunge kwa niaba ya wanafunzi wenzake

Kwa niaba ya wanafunzi wenzake Elieza Richard Chibula amemshukuru mbunge wa Jimbo hilo kwa moyo alioonyesha kujitoa kuwasaidia kutatua changamoto hiyo na kumuahidi kuwa watasoma kwa bidii na kufaulu kwa asilimia 100 katika mitihani ya kidato cha nne mwaka huu dhidi ya asilimi 91 ya ufaulu kwa mwaka 2020.

Mtendaji wa Kata ya Mabula Emmanuel Kimario

Kwa upande wake mtendaji wa kata ya Mabula ambaye aliyepokea mifuko kwa niaba ya wananchi wa Mabula Bw Emmanuel Kimario amesema kuwa msaada huo utasaidia kutatua changamoto waliyo nayo kwani shule ina upungufu wa vyumba viwili vya madarasa ambapo ameeleza kuwa tayari wananchi wameshaanza ujenzi kwa nguvu zao na kwamba ujenzi huo utaghalimu kiasi cha shilingi milion 40 fedha itakayotokana na michango ya wananchi huku akiahidi kuwa atahakikisha hadi mwezi wa pili mwishoni madarasa yanakamilika ili mapema mwezi wa tatu wanafunzi ambao bado hawajaanza masomo waweze kuanza masomo yao mara moja .

Wananchi wa kata ya Mabula wakipokea mifuko ya saruji
 iliyokabidhiwa kwa ajili ya ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa


Wanafunzi wa kidato cha nne shule ya sekondari Mabula wakisalimiana

 kwa furaha na Mbunge wa Jimbo la Kilosa Prof. Kabudi


Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa