• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

KAMATI YA FEDHA , UONGOZI NA MIPANGO IMEFANYA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

Posted on: January 27th, 2024

Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango Wilayani Kilosa ikiongozwa na Mweyekiti wake Mhe. Wilfred Sumari ambaye pia ni diwani wa kata ya Chanzuru  imefanya ziara ya kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo ya Halmashauri hiyo lengo ni kuona utekelezaji wa miradi hiyo na hatua zilizofikia kwa wakati uliokusudiwa kukamilika kwa miradi.

Miradi iliyotembelewa ni Pamoja na Jengo la utawala la halmashauri fedha kutoka serikali kuu mradi utaghalimu kiasi cha bilioni 3,200,000, 000 kukamiliaka jengo lipo hatua ya msingi, Ukumbi wa Halmashauri fedha kutoka mapato ya ndani mradi unakadiriwa  kiasi cha shilingi milioni 922,627,240 kukamilika ambapo mradi huo upo hatua ya ujenzi wa kuta za boma katika kata ya Mabwerebwere.

Sambamba na Shule ya Sekondari Madoto mradi wa SEQUIP fedha kiasi cha shilingi 528,998,425 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa 8, maabara3, jengo la utawala, Tehama, maktaba, matundu ya vyoo 11, kichomea taka na Tank la maji ardhini ambapo ujenzi wa shule hiyo upo hatua ya umalizia katika kata ya madoto.

Pia ujenzi shule ya msingi Mambegwa fedha kiasi cha shilingi milioni 408,900,000 kutoka serikali kuu kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa 7, awali 2, jengo la utwala, nyumba ya walimu, matundu  ya vyoo 18 pamoja na kichomea taka ujenzi upo hatua ya msingi katika kata ya Msowero.

Aidha Ujenzi wa Shule ya Msingi na Awali Dumila juu  mradi wa BOOST kiasi cha shilingi 475,300,000 kwa ajili ya vyumba vya madarasa 14, awali 2, jengo la utawala 1, matundu ya vyoo 18, na kichomea taka ujenzi upo hatua ya umaliziaji  katika kata ya Dumila na Umaliziaji wa bwalo shule ya sekondari Berega kata ya berega ambapo miradi hiyo ya shule ikikamilika itawasaidia wanafunzi kutoka umbali mrefu kufata shule pia kupunguza mrundikano wa wanafunzi wengi madarasani.

Mbali na hiyo miradi mingine iliyotembelea na kamati hiyo ni ujenzi wa stendi ya mabasi dumila ambapo chanzo cha fedha ni mapato ya ndani ya halmashauri ikiwa lengo la mradi huo ni kutoa huduma kwa wasafiri kutoka na Kwenda maeneo mbalimbali Pamoja na wanaingia katika kata ya Dumila.

Aidha kamati hiyo imeipongeza serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuleta fedha kwa ajili ya miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya wilaya ya kilosa ili kuboresha utoaji huduma kwa wananchi.

Akiitimisha Ziara hiyo Mhe. Sumari ameipongeza kamati nzima kwa kusimamia vema shughuli za ujenzi zinazoendelea ambapo baadhi ya miradi ipo hatua ya umaliziaji pia ameitaka kamati kuendelea kusimamia baadhi ya miradi yenye changamoto kutafuta utatuzi wa changamoto hizo ili iweze kutekelezeka kwa wakati kama inavyokusudiwa ingawa changamoto nyingi zimetoakana na hali ya mvua zinazoendelea kunyesha kilosa na kukwamisha zoezi kutofanyika kwa wakati.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa