• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YAFANYA ZIARA YA KUTEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO

Posted on: May 20th, 2024

Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango Wilayani Kilosa imefanya ziara ya kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo ya Halmashauri lengo ni kuona utekelezaji wa miradi hiyo na hatua zilizofikia kwa wakati uliokusudiwa.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo 20 Mei, 2024 mwenyekiti  wa kamati hiyo ambaye pia ni  Diwani wa kata ya Chanzuru Mhe. Wilferd  Sumari ameipongeza timu ya menejimenti  kwa kusimamia vema shughuli za ujenzi zinazoendelea Wilayani hapa huku akiitaka kuendelea kusimamia baadhi ya Miradi yenye changamoto na kuitafutia ufumbazi ili iweze kukamilika kwa wakati kama ilivyokusudiwa ingawa changamoto nyingi zimetokana na hali ya mvua zilizonyesha Wilayani hapa

Miradi iliyotembelewa ni pamoja na Jengo la Utawala la Halmashauri katika kata ya Mabwerebwere fedha kutoka serikali kuu mradi utagharimu kiasi cha shilingi 3,965,145,799.00 kukamilika mpaka sasa mradi upo hatua ya kusimamisha nguzo.

Pia Kamati hiyo imetembelea Ujenzi wa Nyumba ya Mkurugenzi wa Halmashauri iliyopo kata ya Chanzuru. Halmashauri ilipokea kiasi cha shilingi 150,000,000 fedha kutoka serikali kuu ambapo ujenzi upo hatua ya umaliziaji wa kuweka mfumo wa maji safi na maji taka.

Sambamba na shule ya Sekondari Mazinyungu  ambapo fedha kutoka serikali kuu  kiasi cha shilingi 123,000,000.00   kwa ajili ya vyumba vitano vya madarasa na matundu saba ya vyoo mradi huo uliopo kata ya Mkwatani umekamilika. 

 

Aidha Kamati imetembelea ujenzi wa Shule mpya ya Msingi Mambegwa iliyopo kata ya Msowero  fedha kutoka serikali kuu kiasi cha shilingi 408,900,000 kwa ajili ya jengo la utawala 1, vyumba vya madarasa 7,vyumba vya madarasa ya awali 2, matundu 22 ya vyoo, nyumba ya walimu 2 kwa 1,  na  kichomea taka.

Mbali na hayo miradi mingine iliyotembelewa na kamati hiyo ni shule ya sekondari Magole kata ya Magole mradi wa SEQUIP fedha kiasi cha shilingi 25,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa  ujenzi upo hatua ya umaliziaji pamoja na Ujenzi wa Ukumbi wa Halmashauri uliopo kata ya Mabwerebwere fedha kutoka mapato ya ndani ambapo mradi huo umekadiriwa kutumia jumla ya shilingi 922,627,240.00 na kiasi cha shilingi 266,075,000 zimeshatolewa kutekeleza mradi ujenzi upo hatua ya umwagaji wa zege ya nguzo mlalo ya kwanza.

 

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa