• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE TAMISEMI YARIDHISHWA NA MIRADI WILAYANI KILOSA

Posted on: February 20th, 2024

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) ikiongozwa na mwenyekiti wake Mhe. Denis Lazaro Rondo ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Mikumi imeridhishwa na utekelezaji wa ujenzi wa miradi ya “BOOST na SEQUIP” wilayani Kilosa ilipotembelea miradi hiyo Februari 20, 2024.


Akizungumza kwa niaba ya kamati, Mhe. Londo amezipongeza kamati za ujenzi katika miradi hiyo kwa kusimamia vizuri ujenzi wa miradi hiyo.

Kamati hiyo imetembelea na kukagua ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari ya Miwa iliyopo katika kata ya Ruhembe amabayo imejengwa kwa kiasi cha shilingi 528,998,425.00 kwa ajili ya vyumba vya madarasa 8, jengo la utawala 1, maabara 3 ya kemia, bailojia na fizikia, maktaba, chumba cha Tehama, matundu ya vyoo 11, kichomea taka na tanki la maji la ardhini. ambayo imekamilika na imeshaanza kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza kwa upande wa mradi  

Aidha kamati hiyo pia umekagua mradi (BOOST) ujenzi wa shule ya Msingi Ruaha A iliyopo katika kata ya Ruaha uliogharimu kiasi cha shilingi (98,000,000) kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 4 na matundu 6 ya vyoo.

Mhe. Rondo amesema kuwa mradi wa ujenzi wa sekondari mpya ya Miwa imekuwa mkombozi kwa wanafunzi waliokuwa wanatembea zaidi ya kilometa 20 kwenda shule ya jirani kusoma kwani wanafunzi wengi wamekatishwa ndoto zao za kusoma kutoka na vikwazo walivyokuwa wanakutana navyo njiani huku wengi wakibakwa na wengine kupata mimba.


Aidha amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutenga kiasi cha shilingi 528,998,425.00 kwa ajili ya ujenzi wa shule hiyo pamoja na miradi mingine ndani ya kata hiyo kama vile ujenzi wa Daraja Ruhembe linalojengwa kwa thamani ya shilingi zaidi ya bilioni moja.

Naye mbunge wa jimbo la Kilosa Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi amewaasa wananchi wa Ruhembe kuitunza miundombinu ya shule hiyo huku akiwataka wanafunzi kusoma kwa bidii kwani miondombinu na mazingira ya shule hiyo ni rafiki kwao kujipatia elimu iliyo bora.

Pia mbunge wa viti maalum kutoka mkoa wa Tabora Mhe. Hawa Subira Mwaifunga ambaye pia ni mjumbe wa kamati hiyo amewataka watendaji kusimamia vizuri miradi mbalimbali inayoendelea kutekelewa wilayani humo.

Sambamba na hayo Mbunge wa jimbo la Hai Mhe. Sashisha Herinikyo Mafue ambaye pia ni mjumbe wa kamati hiyo amewapongeza wananchi wa jimbo la la Mikumi kwa kumchagua Mhe. Rondo kuwa mbunge wao kwani amekuwa msaada mkubwa kwa jimbo hilo na serikali kwa ujumla hususani katika kuiongoza kamati hiyo kwa weredi mkubwa.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe. Shaka Hamdu Shaka ameishukuru kamati hiyo kwa kuitembelea wilaya ya Kilosa na kujionea utekelezaji wa miradi mbalimbali huku akiwaahidi wanakamati na wananchi kwa ujumla kuendelea kuitunza miradi hiyo Pamoja na kuisimamia miradi mingine inayoendelea kutekelezwa wilayani humo.

Aidha mh. Shaka ameahidi kuwa hatowafumbia macho baadhi ya watendaji, wahandisi pamoja na wakandarasi wataoshindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo katika ujenzi na usimamizi wa miradi hiyo kwani serikali ya awamu ya sita imejizatiti kuwaletea huduma wananchi wake.

Akihitimisha ziara hiyo Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo amabaye pia ni mbunge wa jimbo la Kilolo mkoani Iringa Jastin Lazaro Nyamoga ametoa pongezi kwa wasimamizi wa miradi hiyo akiwemo mkuu wa Wilaya pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri kwa kuisimamia miradi hiyo kwani inakidhi ubora unaotakiwa.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa