• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

Kamati ya Siasa Wilaya yapongeza kazi zilizofanyika kwenye miradi

Posted on: April 23rd, 2021

Katika kuhakikisha ilani ya uchaguzi ya chama tawala (CCM) inatekelezwa katika ngazi ya wilaya Kamati ya Siasa Wilaya imetembelea miradi mbalimbali katika jimbo la Kilosa na Mikumi ili kujionea namna ilani hiyo inavyotekelezwa katika kuwaletea maendeleo wananchi.

Kamati hiyo imefanya ziara ya siku mbili katika jimbo la Kilosa na Mikumi Aprili 22 hadi 23 mwaka huu ambapo katika imetembelea miradi katika sekta ya elimu, maendeleo ya jamii, maji na afya ambapo imepongeza juhudi kubwa zinazofanywa na uongozi wa Halmashauri pamoja viongozi wa kata kwa namna ambavyo wameshirikiana sambamba na wananchi katika kujiletea maendeleo.

Akiongelea miradi iliyotembelewa Katibu wa CCM Wilaya ya Kilosa Abdallah Mdimu amesema wamejionea kazi kubwa iliyofanywa huku wakipongeza kuwa miradi hiyo inalingana na kiwango cha thamani ya fedha kilichotumika ambapo pia amesisitiza watumishi wote katika sekta hizo kufanya kazi kwa uzalendo kwa ajili ya taifa lao.

Aidha kamati hiyo kwa imepongeza juhudi kubwa zilizofanywa katika kituo cha afya Mikumi kwa huduma kubwa mbili za upasuaji zilizopelekea kuokoa maisha ya mama na mtoto ambazo zilifanyika kwa ufanisi na ushujaa mkubwa huku wakisisitiza kuwepo kwa uzio katika vituo vyote vya afya ili kulinda mipaka huku upande wa elimu wakitaka shule zilizotembelewa kuwa na mpango wa mabweni kipaumbele kikiwa kwa watoto wa kike ili kuwaepusha na vishawishi wanavyoweza kukumbana navyo ikiwemo mimba.

Pamoja na hayo kamati hiyo imeitaka Halmashauri na idara husika kuvisimamia kwa ukaribu vikundi vyote vilivyochukua mikopo na bado havijarejesha kuhakikisha vinafanya hivyo ikiwemo kuvisaidia kwa kuvisimamia ili vitumie mikopo hiyo kikamilifu na kitaalam kwa lengo la kupata tija na kurejesha fedha ili vikundi vingine viweze kukopa huku wakisisitiza vikundi vilivyokopa kurejesha mikopo kwa wakati.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kilosa  Alhaji Adam Mgoyi amemuagiza mtendaji wa kata ya Ruaha kukisimamia kikundi cha walemavu kilichopo katika kata ya hiyo kwa kuhakikisha kinavuniwa miwa yake ambayo ipo tayari kwa kuvunwa ili kivuniwe na kufanya mauzo ambayo yatakiwezesha kupata fedha na kuanza kurejesha mkopo ambao kimepatiwa na Halmashauri kwa mujibu wa sheria na taratibu.

Katika ziara hiyo miradi mbalimbali ya ujenzi na ukarabati imetembelewa katika ni shule za sekondari Mikumi, Ukwiva, Dakawa na Kilosa, shule za msingi za Lumango, Ujirani, Msowero na Matongolo huku upande wa maendeleo jamii vimetembelewa kikundi cha walemavu kilichopo katika kijiji cha Kifinga, kikundi cha kinamama Mvumi na kikundi cha vijana kinachojishughulisha na mradi wa kutengeneza chaki kilichopo kata ya Magole na upande wa afya kituo cha Afya Mikumi, Dumila na Mvumi pamoja na mradi wa maji uliopo kata ya Kitete.


Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa