• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

KAMATI YA ULINZI NA USALAMA KILOSA YAMZAWADIA OC CID LESIO KWA KUKATAA RUSHWA

Posted on: April 9th, 2020

Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Kilosa imemzawadia OC CID wa Wilaya ya Kipolisi ASP Onesphory Lesio zawadi ya shilingi 100,000/ ikiwa kama pongezi kwake kwa kitendo cha uzalendo na kishujaa alichokionyesha kwa kukataa rushwa ya shilingi 340,000/= toka kwa watuhumiwa ambao kesi yao ilikuwa mahakamani ili awasaidie na kuwaachia baada ya kukutwa na biashara haramu ya madawa ya kulevya.

MKUU WA WILAYA AMBAYE NI MWENYEKITI WA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA ADAM MGOYI AKIMKABIDHI OC CID ONESPHORY LESIO ZAWADI YA SHILINGI 100,000/

Zawadi hiyo imetolewa Aprili 9 mwaka huu na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi Aprili 8  tukio hilo lilishuhudiwa na kamati ya Ulinzi na Usalama katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ambapo Mkuu wa Wilaya amesema OC CID huyo ameonyesha kitendo cha uzalendo kwani kwa nafasi yake alikuwa na nafasi nzuri ya kupokea rushwa hiyo lakini kutokana na kuithamini kazi yake hakupokea rushwa ambayo inapoteza haki za watu na kusababisha uonevu ambapo OC CID huyo baada ya ushawishi huo wa kupokea rushwa alitoa taarifa kwa taasisi ya kupambana na rushwa (TAKUKURU) ambao walifanikisha kukamatwa kwa watuhumiwa baada ya kuweka mtego uliowanasa watuhumiwa.

Mgoyi amesema kuwa kitendo kilichofanywa na OC CID ni kitendo cha uzalendo kwani Wilaya ya Kilosa imekuwa ni mhanga wa matendo ya rushwa lakini kutokana na mabadiliko ambayo viongozi wamekuwa wakionyesha kwa kukemea vitendo vya rushwa kwa vitendo hivyo kamati ya Ulinzi na Usalama kwa kuunga mkono kitendo cha kizalendo imemzawadia kiasi hicho cha fedha huku akisema mfano huo uwe ni wa kuigwa kwani anaamini jeshi la polisi ni chombo chenye uadilifu hivyo waige kutoka kwa kiongozi huyo na kwamba kila mwananchi anaowajibu wa kumuunga mkono Rais wa awamu Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kupinga vitendo vya rushwa.


Naye Mkuu wa TAKUKURU Wilaya ya Kilosa Lawrance Mlaponi amesema baada ya kupata taarifa kutoka kwa OC CID walifanikisha kuwakamata watoa rushwa na kwamba TAKUKURU inatoa wito kwa watumishi wa umma kutojihusisha na vitendo vya rushwa ili kutotekeleza majukumu yao huku akisisitiza wananchi kutotoa rushwa kwa watumishi ili kupata haki wasiyostahili ama upendeleo na kwamba yoyote anayejihusisha na masuala ya rushwa TAKUKURU haitasita kuwakamata na kuwafikisha katika vyombo vya dola.

OC CID ONESPHORY LESIO AKISHUKURU KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA KILOSA.

Akielezea tukio hilo OC CID ASP Onesphory Lesio amesema watuhumiwa baada ya kuona kesi yao iko mahakamani na ndugu zao wameshafikishwa kwenye vyombo vya dola walikusudia kutoa rushwa ili aweze kuwasaidia ambapo kutokana na uzalendo na uadilifu alitoa taarifa TAKUKURU ambao walitoa ushirikiano na kufanikisha kukamatwa kwa watuhumiwa pia amesema anawashukuru TAKUKURU kwa namna walivyotoa ushirikiano na kusema kuwa Jeshi la Polisi limedhamiria kupinga vitendo hivyo kwani awali Jeshi la Polisi lilikuwa likikataa vitendo vya rushwa pasipo kukamata wahusika lakini kwa sasa linakemea vitendo hivyo kwa kuhakikisha wanawakamata watuhumiwa kwa kuwashirikisha TAKUKURU hivyo kila mmoja ashiriki kwa nguvu zote kukemea vitendo vya rushwa.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa