• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

KAMATI ZA UKIMWI NGAZI YA WILAYA/KATA ZAPATIWA MAFUNZO

Posted on: June 13th, 2019

Imeelezwa kuwa serikali kwa kiasi kikubwa imeweza kuweka mifumo mbalimbali ya utoaji huduma za afya na ustawi wa jamii zikiwemo kamati shirikishi za ukimwi katika jamii na kamati mbalimbali licha ya uwepo wa changamoto mbalimbali kama vile ukosefu wa fedha na mafunzo na kusababisha kutofikia malengo yaliyokusudiwa.

Hayo yameelezwa na Afisa Maendeleo ya Jamii na Mratibu wa Ukimwi Mkoa Bi. Ndayakundwa Henry wakati wa mafunzo kwa timu ya uwezeshaji na uratibu wa kamati za ukimwi ambapo amesema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwezesha Halmashauri na kata kuboresha mifumo ya huduma za afya na ustawi wa jamii kupunguza maambukizi na madhara ya virusi vya UKIMWI kwa makundi maalum, kujengea uwezo wa uratibu, ushawishi na utetezi kwa masuala ya UKIMWI kwa jamii na kuwezesha masuala ya usimamizi shirikishi wa kamati za kudhibiti UKIMWI za kata ziweze kutekeleza majukumu yake.

Licha ya kubainisha malengo ya mafunzo hayo Mkurugenzi wa JSI Kanda ya Pwani Pamela Msei amesema kuwa kamati hizo zinao wajibu na  majukumu ya kuhakikisha kamati za VVU na UKIMWI zinaundwa na kufanya kazi kwa kila ngazi kwa kufuata miongozo, kuhakikisha tathmini ya hali halisi ya VVU na UKIMWI katika Halmashauri inafanyika na kuweka mikakati ya utekelezaji kila mwaka, kuhakikisha mipango yote ya UKIMWI na wadau wanaotekeleza katika Halmashauri husika vinaingizwa kwenye mpango mkakati wa Halmashauri na mkoa kuondoa urudufu wa juhudi za rasilimali sambamba na kuhakikisha sheria ndogo, mkakati wa Taifa wa kudhibiti UKIMWI, sheria, miongozo na matokeo ya tafiti mbalimbali ya masuala ya UKIMWI yanawafikia wadau na wananchi kwa ujumla.

Naye Mratibu wa UKIMWI wilaya ya Kilosa Emeresiana Temu amesema kuwa programu ya uimarishaji mifumo ya afya ya jamii na ustawi wa jamii kwa kamati za ukimwi ngazi ya kata yanaendelea chini ya halmashauri yakifadhiliwa na shirika la jsi research katika kata tano ambazo ni Magomeni, Kasiki, Mbumi, Mkwatani na Mabwerebwere lengo ikiwa ni kuhakikisha kamati hizo zinafanya kazi na kuwasilisha taarifa zao kwa mratibu kila robo ya mwaka ambapo kamati hizo zitafanya kazi ya kujua hali ya maambukizi ya VVU/UKIMWI kupitia kata zao na kutengeneza mikakati ya namna ya kutokomeza kuwepo kwa maambukizi mapya.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa