• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

KILOSA HALI NI SHWARI HAKUNA MAFURIKO

Posted on: November 19th, 2023

Licha yaTahadhari zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali juu ya uwepo wa mvua kubwa za Elnino kutoka mamlaka ya hali ya hewa Nchini, wakazi wa wilaya ya kilosa  wanaoishi sehemu za mabondeni na pembezoni mwa mito wameendelea  kupewa tahadhari ya kuhama ili kuepusha madhara makubwa.

 Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe. Shaka Hamdu Shaka amesema hayo novemba 19,2023 wakati wa  ziara ya kutembelea na kukagua mito  na mifereji inayotiririsha maji wilayani hapa na kusema kuwa  hali ya mito hiyo pamoja na mifereji ni shwari na hakuna dalili wala viashiria vya mafuriko kama ambavyo inadhaniwa na baadhi ya Watu,hii ni baada ya  video fupi kusambaa kwenye mitandao ya kijamii ikionesha mafuriko na mifugo kusombwa na maji jambo ambalo si sahihi.

Mhe. Shaka ameeleza kuwa kamati ya ulinzi na usalama imetembelea na kukagua kwa mito na mifereji inayotiririsha maji na kubaini kuwa kipimo cha maji kwenye mito hiyo ni 0.42 ambacho ni kiwango cha kawaida na kuongeza kuwa wataendelea kufatilia jambo hilo kwa ukaribu lengo likiwa ni kuhakikisha na kuwa Wanachi wa kilosa na mali wako salama.

Mhe Shaka amewaonya Watu wenye tabia ya kutoa taarifa ambazo hawana uhakika kwani  zinaweza kuibua taharuki katika jamii na kusabisha hali ya uvunjivu wa amani na usalama kwa wakazi wa eneo husika.

Samba samba na hayo Shaka amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassani kwa kuipatia Halmasahuri ya Wilaya ya Kilosa fedha kiasi cha shilingi Bilioni 13 kwa ajili ya ujenzi wa miundo mbinu za barabara na mifereji ya kisasa inayotiririsha maji na kuizuia kuingia kwenye makazi ya wananchi.

Kwa upande wake  Afisa Mazingira wa Wilaya ya Kilosa Ndg. Anthony Heri Mbise amesema kuwa Elimu bado inaendelea kutolewa juu ya kuchukua tahadhali kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali na kuwataka kuchukua taadhali ili kuepuka madhara yanayoweza kujitokeza.

Mbise ameongeza kuwa vikundi mbalimbali vimeundwa ikiwemo Kamati ya maafa kwa ajili ya kupeana taarifa endapo kuna mabadiliko au viashiria vya kuwepo na mafuriko na kwamba  mpaka sasa hakuna taarifa yoyote inayoeleza kuna mabadiliko ya hali ya hewa au  mafuriko.

   

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa