• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

KILOSA KUANDAA MPANGO WA UWEKEZAJI ILI KUINADI WILAYA

Posted on: March 6th, 2020

Washiriki kutoka Halmashauri ya wilaya ya Kilosa na wadau mbalimbali katika uandaaji wasifu wa Wilaya ya Kilosa wametakiwa kushiriki kikamilifu katika kubaini sekta mbalimbali za uwekezaji wakiwa na taarifa sahihi za sekta mbalimbali ikiwemo kilimo, ufugaji sambamba na kubainisha ukubwa wa ardhi tuliyonayo kwa ajili ya kilimo na ufugaji kama wilaya.

Wito huo umetolewa na  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Asajile Mwambambale ambapo amesema washiriki wanapaswa kutoa taarifa na takwimu mbalimbali wanazozifahamu jambo litakalosaidia zoezi la uandaaji wa mpango wa uwekezaji/ wasifu waWilaya  Kilosa chini ya uwezeshaji wa programu ya  ENGINE ambao wameleta wataalam washauri (consultants) toka nje na ndani ya nchi ambapo kupitia uwezeshaji wao na taarifa zitakazotolewa  zitasaidia kwa kiasi kikubwa  kupata mpango wa uwekezaji ili kuitangaza wilaya yetu katika sekta ya uwekezaji.

Aidha amesema kuwa pamoja na kubainisha taarifa na takwimu mbalimbali hususani katika sekta ya kilimo na mifugo pia ametoa wito kwa washiriki hao kutoishia katika kubainisha taarifa hizo bali nao wawe ni sehemu ya kuzitumia sekta hizo badala ya kuwaachia wawekezaji toka nje kwani na wao wana nafasi ya kuwekeza kwani fursa ziyo na inawezekana kuwekeza kwa maslahi yao na wilaya kiujumla.

BAADHI YA WASHIRIKI WA UANDAAJI MPANGO WA UWEKEZAJI

Pamoja na hayo ameeendelea kusisitiza kuwa kazi ya uandaaji mpango wa uwekezaji ni kwa maslahi ya wilaya yetu ili kuweza kuleta tija ambapo amenadi wilaya ya Kilosa ina miji ya Mikumi,  Dumila,  Ruaha na Kilosa ambayo inaweza kuchangia kukua kwa sekta ya biashara huku akinadi kuwa Wilaya imebarikiwa kuwa na maji mengi ambayo yanaweza kutumika katika kilimo cha umwagiliaji lakini pia uwepo wa ujenzi wa reli ya mwendo kasi (SGR) ambayo Kilosa inatarajiwa kuwa mojawapo ya stesheni kubwa ambapo ametaka uwepo wa stesheni hiyo kutumika kama fursa ya uwekezaji na kwamba uandaaji mzuri wa mpango wa uwekezaji ndio chanzo cha kuvuta wawekezaji kwa wingi zaidi.

BW. ANTONY JONES TOKA KAMPUNI YA AJC MTAALAM WA MIPANGO KATIKA SERIKALI ZA MITAA TOKA MAREKANI

BW. GALINOMA LUBAWA MHADHIRI FEDHA ZA MAENDELEO NA UWEKEZAJI

BW.KELVIN KALEGEYA MWAKILISHI WA PROGRAMU YA ENGINE MKOA WA MOROGORO


Mwambambale pia amewasihi wataalam kutoka ENGINE kwa ajili ya uandaaji wa mpango wa uwekezaji kutosita kuelekeza njia njema ili mchango wao uweze kusaidia mpango wetu kukaa vizuri kwani tuna mambo mazuri yanayoweza kuwa na uwekezaji mzuri na kuitangaza Kilosa kwa ajili ya uwekezaji ikiwemo uwepo wa barabara kubwa ya iliyopita wilayani Kilosa inayounganisha barabarab mbili kubwa za Morogoro - Dodoma mpaka Mwanza na Morogoro - Iringa mpaka Zambia ambayo inapita kutoka Dumila kwenda Mikumi inaweza kuwa kivutio kwa wawekezaji kuona fursa mbalimbali na kuzichangamkia.

.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa