• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

KILOSA KUMKOMBOA MTOTO WA KIKE KWA KUJENGA SHULE MAALUM YA WILAYA YA BWENI

Posted on: September 17th, 2020

Katika kuhakikisha changamoto mbalimbali zinazowakabili wanafunzi hususani wa kike na kusababisha kutofikia malengo yao kielimu Halmashauri ya wilaya ya Kilosa imeazimia kujenga shule ya sekondari ya bweni kwaajili ya watoto wa kike kwa kutumia fedha za mapato ya ndani ya halmashauri, michango ya wananchi na kwa wadau wa maendeleo.

Hayo yamebainishwa Septemba 17 mwaka huu na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Asajile Mwambambale wakati wa kikao maalum kilichoshirikisha kamati ya ulinzi na usalama, timu ya menejimenti, maafisa tarafa, watendaji wa kata na vijiji pamoja na wenyeviti wa vijiji na ambapo Mgeni rasmi wa kikao hicho akiwa Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mh Adam Mgoyi.

Mwambambale amesema kuwa katika safari ya kutafuta elimu watoto wa kike wamekuwa wakikabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo mimba za utotoni kutokana na kutembea umbali mrefu kwenda shule, kuozeshwa, kurubuniwa na wanaume hali ambayo imekuwa ikiwarudisha nyuma katika kutimiza malengo yao  na kusema kuwa ndiyo maana wamekuja na mpango huo wa kujenga shule ya bweni ili ikawe mkombozi wa wanafunzi wa kike.

Mwambambale amesema mpango huo unatarajiwa kutekelezwa haraka iwezekanavyo  huku ikitarajiwa ifikapo mwaka 2021 wanafunzi wa kidato cha kwanza waanze kusoma katika shule hiyo na kwamba tayari maandalizi ya awali ya ujenzi wa shule hiyo yamekwishaanza  ambayo mpaka kukamilika kwake itatumia shilingi milioni 861 na huku  zoezi la ufyatuaji tofali likianza Septemba 18 mwaka huu.

 Aidha amesema shule hiyo itajengwa katika eneo la Kondoa katika kata ya Mabwerebwere ambapo kuna eneo la hekari 16 na tayari tripu 60 za mchanga na saruji mifuko 1,800  vimeshapelekwa katika eneo la mradi tayari kwa kazi ambapo  amewataka viongozi hao kuweka nguvu ya pamoja katika kuhamasisha wananchi na wadau mbalimbali kuchangia ujenzi huo kwaajili ya kumkomboa mtoto wa kike wa Wilaya ya Kilosa.

Nao viongozi hao wamepokea suala hilo kwa mikono miwili na kuupongeza uongozi kwa maono mazuri waliyonayo katika sekta ya elimu huku wakiahidi wao binafsi kuwa mstari wa mbele kwa kuchangia na kuhamasisha wananchi katika kuchangia ili ujenzi wa shule hiyo uweze kukamilika kama ilivyopangwa.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa