• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

KILOSA KUWA MFANO WA KUIGWA KATIKA MAPINDUZI YA SEKTA YA MIFUGO

Posted on: January 4th, 2025

Katika kuhakikisha sekta ya mifugo na uvuvi inasonga mbele kwa kasi Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji amesema Serikali ya awamu ya sita imetoa fedha kiasi cha Shilingi Bilioni 28 .1 kwa ajili ya mapinduzi katika sekta hiyo ili kuleta mabadiliko kwa kuwa na ufugaji wenye tija nchini.

Dkt. Ashatu ameyasema hayo 3 Januari , 2025  wakati akizindua mashamba ya malisho ya mifugo  katika Vijiji vya  Mandela na Mbwade  Wilayani kilosa ambapo amesema kuwa mkoa wa morogoro  unakwenda kuwa mfano wa kuigwa kwa kufanya ufugaji wa kisasa utakaopelekea kuondoa migogoro ya wafugaji na wakulima pia kuongeza  masoko  nje ya nchi na kuinua uchumi kwa wafugaji.


Dkt. Ashatu ameongeza kuwa wafugaji wote wanatakiwa kuwa na maeneo ya malisho sambamba na visima vya maji, kuwapatia chanjo mifugo yao pamoja na utambuzi wa mifugo ili kupata takwimu sahihi zitakazosaidia kufanya mipango ya maendeleo.

Sambamba na hayo Waziri  Ashatu ameeleza kuwa serikali itafanya maboresho kwa kutoa vitendea kazi ambapo maafisa ugani watanunuliwa pikipiki mia saba (700 ) na vishkwambi elfu nne mia tano (4500) ambapo kupitia vitendea kazi hivyo  vitawarahisishia maafisa ugani hao kuweza kufanya kazi kwa weredi na kuondokana na changamoto ya usafiri na utunzaji wa takwimu kidigitali.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amewataka Maafisa Watendaji wa kata na Vijiji kuacha kufanya tathmini ya ulishwaji wa mazao isiyo ya kweli na kupelekea kumuonea mkulima na badala yake wafanye tathmini ya kweli ili mkulima alipwe kulingana na kile alichopoteza.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe. Shaka Hamdu Shaka amesema kuwa kwa kipindi cha miaka mitatu asilimia kubwa wilaya ya kilosa imepunguza vifo vinavyotokana na migogoro ya Wakulima na wafugaji kutokana na njia mbalimbali zilizokuwa zikifanywa na vyombo vya ulinzi na usalama.

Pia chifu Matayane Simanga ambaye ni chifu wa wamasai ameshukuru kwa ujio wa Mhe. Waziri na kuahidi kuyafanyia kazi maelekezo  yaliyoongelewa na kusema kuwa wataendelea kuhamasisha jamii za wafugaji kufuata njia za ufugaji wa kisasa ili kuepukana na migogoro ya wakulima na wafugaji.

Tangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA WAHE. MADIWANI May 22, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • WAUGUZI WATAKIWA KUWA WAADILIFU MAHALI PA KAZI

    May 30, 2025
  • WAHE. MADIWANI WAISHUKURU SERIKALI YA AWAMU YA SITA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    May 30, 2025
  • KILOSA YAJIPANGA KUTATUA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI

    May 28, 2025
  • VITENGO VYA HABARI SERIKALINI VIIMARISHWE KWA KUFANYA MAWASILIANO YA KIMKAKATI

    May 24, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa