• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

Kilosa yaadhimisha miaka 59 ya Muungano kwa kupanda miti

Posted on: April 26th, 2023

Katika kuadhimisha miaka 59  ya Muungano wa Tanganyika za Zanzibar Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mh Shaka H. Shaka ametoa rai kwa wanakilosa kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika uhifadhi wa mazingira ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

Rai hiyo imetolewa  Aprili 26 mwaka huu wakati wa zoezi la upandaji miti katika eneo la mto Mkondoa ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 59 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambapo amesema kuwa Serikali imekuwa ikikabiliana na mabadiliko ya tabia nchi kwa kuhakikisha mazingira yanahifadhiwa kwa njia mbalimbali ikiwemo ya kupanda miti  nyakati zote na kwamba kwa mwaka 2022/23 Wilaya ya Kilosa inapaswa kupanda miti ipatayo 1,500,000.  


Licha ya mabadiliko ya tabia nchi Mh. Shaka amesema kumekuwa na tabia ya ukataji mito na kutothamini misitu jambo ambalo si sahihi, hivyo kila mmoja anao wajibu wa kutunza mazingira kwa kufanya jitihada za upandaji miti kuwa zoezi endelevu na kwamba hadi sasa wilaya imefanikiwa kupanda miti  789,000, pia amewataka viongozi wa kata na vijiji kujiwekea malengo ya upandaji miti kuanzia ngazi ya kata kupanda miti takribani 500 kwa mwezi jambo litakalosaidia kufikia malengo yaliyowekwa na Serikali huku akizitaka taasisi zilizopo Kilosa kushiriki katika kampeni ya upandaji miti sambamba na utoaji elimu wa namna ya utunzaji miti yote inayopandwa na ambayo imeshapandwa.


Pamoja na hayo amewataka wanakilosa kufahamu kuwa Muungano umekuwa na mafanikio mbalimbali ndani ya nchi ikiwemo mwingiliano wa kimahusiano baina ya Tanzania bara na visiwani, uwepo wa amani, uendelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati, kufunguka kwa nyanja za kiuchumi na kwamba watanzania tunayo kazi ya ya kuulinda Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kama tunu ya Taifa ili kulifanya Taifa kuwa lenye umoja na mshikamano.

Kwa upande wake Katibu Tawala Yohana Kasitila amesema upandaji miti umefanyika katika mto Mkondo kwa lengo la kuendeleza utunzaji wa mto huop ili kuondoa adha ya mafuriko kwani mara nyingi mto huo umekuwa ukikumbwa na mafuriko na kwamba kampeni ya upandaji miti itakuwa endelevu katika mito mingine iliyopo wilayani Kilosa.

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa upandaji miti Afisa Maliasili Sadala Ally amesema zoezi la upandaji miti kwa Wilaya ya Kilosa ni endelevu ambalo linashirikisha wadau mbalimbali ambapo ili kukabiliana na changamoto za uchomaji moto, kung’olewa kwa miti hovyo, miti kuliwa na mifugo wakati wa kiangazi halmashauri imejipanga kuendelea kutoa elimu ya mazingira  kwa jamii, uanzishaji wa klabu za mazingira mashuleni, kuunda, kusimamia  na kuboresha kamati za maliasili, kutoa elimu ya utunzaji vyanzo vya maji, kuhamasisha Serikali za vijiji kusimamia miti iliyopandwa na kukuendelea kutenga bajeti ili kuwezesha shughuli za upandaji miti.



Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa