• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

KILOSA YAELEZA NAMNA INAVYOTEKELEZA ILANI YA UCHAGUZI

Posted on: March 4th, 2020

Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa imeendelea kutekeleza ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi kwa kipindi cha mwaka 2018/2019 ambao unakwenda sambamba na falsafa ya Serikali ya awamu ya tano ya hapa kazi tu lengo ikiwa ifikapo mwaka 2025 kuwe na Taifa lenye maisha bora kwa kila mtanzania.

Katibu Tawala Wilaya Yohana Kasitila amebainisha hayo Machi 3 mwaka huu alipokuwa akisoma taarifa ya utekelezaji wa ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya 2015- 2020 kwa kipindi cha mwezi Julai 2018 hadi Disemba 2019 kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya katika kikao cha Halmashauri kuu ya CCM Wilaya ambapo amesema taarifa hiyo imetekeleza kwa vitendo ahadi zilizotolewa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Joseph Pombe Magufuli  ambayo inatoa dira ya utekelezaji Sera za Serikali kwa kuzingatia masuala ya msingi.

Akieleza masuala hayo Kasitila amesema mojawapo ya mambo hayo ni kujenga uchumi wa kisasa wa taifa linalojitegemea kwa kusimamia kikamilifu ukusanyaji wa mapato ya ndani, kuwawezesha wananchi kiuchumi ili waweze kumiliki na kuendesha uchumi na kipato kwa wananchi  pamoja na kujenga viwanda vikubwa, vya kati na vidogo kwa lengo la kukuza uchumi na kuongeza ajira kwa wananchi hasa vijana.

Kasitila amesema kuwa katika utekelezaji huo Halmashauri imetekeleza shughuli mbalimbali ikiwemo utekelezaji wa utoaji asilimia kumi ya mikopo kwa wanawake,  vijana na watu wenye ulemavu  kwa 2018/2019 shilingi 221,114,629.00 kwa vikundi 51, mwaka wa fedha 2019/2020 hadi kufikia Disemba 2019 jumla ya shilingi 180,099,842.08 kwa vikundi 26 ambapo pia Halmashauri imejiwekea mkakati kuhakikisha kwa kila mapato ya ndani yanayopatikana asilimia 10 lazima itengwe na kupelekwa kwa vikundi hivyo.

Aidha upande wa sekta ya afya Halmashuri imekamilisha ujenzi wa kituo cha afya Mikumi ambapo pia kimeanza kutoa huduma kwa wagonjwa wa nje ambapo pia amesema ujenzi katika vituo vya afya Malolo na Mvumi unaendelea  wakati huo katika kuhakikisha uzazi salama wa mama mjamzito na mtoto unakuwepo Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa  imeanza kutoa huduma katika wodi mpya ya wazazi kwa kiwango kinachoridhisha tofauti na jengo la awali ambalo miundombinu yake ilikuwa hairidhishi.

Kwa upande wa sekta ya elimu ili kuhakikisha wanafunzi wanakuwa na mazingira bora ya kufundishia na kujifunzia Serikali imeendelea kuleta pesa ili kuboresha miundombinu ya kujifunzia na kufundishia ikiwa ni pamoja na kujenga miundombinu mipya , kukarabati na kufanya umaliziaji wa miundombinu iliyoanzishwa na wananchi katika maeneo mbalimbali huku upande wa sekta ya uchumi (kilimo na umwagiliaji) kwa kuhakikisha mnyororo wa thamani ya mazao kwa wakulima unaongezeka ambapo Serikali imetoa shilingi 971,311,119.00 kwa ajili ya ujenzi wa ghala la kuhifadhia mazao Mvumi.

Licha ya hayo  katika sekta ya maji Halmashauri imetoa shilingi 70,000,000.00 kutoka katika mapato yake ya ndani ikiwa ni utekkelzaji wa agizo la Mheshimiwa Waziri Mkuu katika eneo la Ruaha kwenda kwenye akaunti ya RUWASA ambapo hadi sasa mradi umetekelezwa kwa 80%.

 Kasitila amesema mchango wa Halmashauri katika utekelezaji shughuli za maendeleo imekuwa ikichangia kwa kiasi kikubwa katika mwaka wa fedha 2018/2019 jumla ya shilingi 1,097,454,134.93 zilielekezwa katika shughuli za maendeleo huku Julai hadi Disemba shilingi 632,426,640.97 zikielekezwa katika shughuli za maendeleo

Katika utekelezaji huo Kasitila amesema zipo changamoto mbalimbali zilizojitokeza ikiwemo migogoro ya wakulima na wafugaji iliyosababisha uharibifu wa mali, binadamu, mifugo na mazao, baadhi ya skimu za umwagiliaji kushindwa kutumika kikamilifu kipindi cha kiangazi kutokana na mifugo ya wafugaji kuvamia mashamba ili kufata malisho na maji, athari za mafuriko katika kata mbalimbali na kusababisha uharibifu wa miundombinu ya kitaifa ya Reli ya Kati na barabara kuu hususani barabra za Mikumi-Kilosa-Dumila, Kilosa-Melela-Morogoro na Morogoro-Dumila-Dodoma pamoja na uhaba wa watumishi katika kada mbalimbali hususan sekta ya afya, elimu na maendeleo ya jamii.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa