• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mipango
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mifungo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

Kilosa yaendelea kutambua juhudi za Serikali kwa Watumishi wa Umma na Wananchi-DED Kilosa

Posted on: December 19th, 2022

Katika kukabiliana na changamoto ya uhaba wa vyombo vya usafiri Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa  kupitia bajeti ya  mwaka wa fedha 2021/2022 ilifanikiwa kununua magari mawili kwa kutumia fedha za mapato ya ndani ili kupunguza adha ya changamoto hiyo ingawa upungufu bado ni mkubwa.

Hayo yamebainishwa Desemba 19, 2023 na Mkurugenzi Mtendaji wa wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Kisena Mabuba Mkurugenzi wakati akitoa taarifa ya Halmashauri mbele ya Waziri  wa Nchi, Ofisi ya Rais  Manenimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mh. Jenista Mhagama wakati wa ziara yake ya siku moja ambapo alizungumza na watumishi wa Umma katika ukumbi wa Chuo cha Ualimu Ilonga.

Mabuba amesema kuwa  licha ya ununuzi wa magari hayo pia amesema Halmashauri imetenga bajeti ya kununua magari mengine mawili, na kwamba katika bajeti ya mwaka huu  imepanga kununua  pikipiki 40 kwaajili ya watendaji wa kata ili ziwasaidie katika utendaji kazi kwani kata nyingine ziko umbali wa zaidi ya kilometa 300 mpaka kufika makao makuu ya Wilaya.

Sambamba na hayo ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kazi kubwa inayoendelea katika kupunguza malalamiko na kero za watumishi  ambapo amesema  Halmashauri kwa mwaka huu wa fedha  imepokea watumishi wapya 198 katika kada mbalimbali kwa kiasi kikubwa watasaidia kutoa huduma kwa wananchi.

Aidha amesema kuwa Halmashauri inaendelea kutatua kero za watumishi zilizo ndani ya uwezo na zile ambazo ziko nje ya uwezo zinapelekwa mahala panapohusika ili ziweze kutatuliwa huku  akisema katika  mwaka wa fedha ulioisha takribani watumishi 800 wa kada mbalimbali  wameweza kupandishwa madaraja na vyeo pia kulipwa malimbikizo mbalimbali ya madeni ikiwa ni hatua kubwa iliyofanywa na Serikali.

Akieleza mafanikio ya Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini Awamu ya Tatu(TASAF) Mratibu wa TASAF Wilaya Dedan Maube amesema wanafunzi 10,705 kutoka katika kaya za walengwa wananufaika na ruzuku ya masharti ya elimu hivyo kupelekea kuinua mahudhurio yao hadi kufikia zaidi ya asilimia 90 huku watoto 1988 kutoka katika kaya za walengwa wananufaika na ruzuku ya masharti ya afya lakini pia            Mpango umeweza kuvifikia vijiji vyote 138 na mitaa 18 ya Wilaya ya Kilosa ambapo kaya 10572  zinanufaika na mpango huku miradi ya Visima 14 ikitekelezwa na mtandao wa maji bomba katika vijiji vya Makwambe, Manzese, Madudumizi, Nyangala, Ilakala na Rudewa Mbuyuni kupitia Miradi ya ajira za muda  kuwasaidia akina Mama na watoto ambapo wameupukana na adha ya kutembea umbali mrefu kutafuta maji na pia kuepukana na magonjwa yanayohusiana na kunywa maji yasiyo salama ya mito.

Maube amesema ujenzi wa vivuko na mitaro ya kutiririsha maji umesaidia kuondoa mafuriko kwenye makazi ya wananchi katika vijiji vya Rose, Behewa, Kiyangayanga, Mbwamaji, Ruaha, Tundu na Mtumbatu lakini pia utekelezaji wa miradi ya Miti umewezesha uboreshaji wa mazingira yalioharibiwa na shughuli za kibinadamu na imesaidia kurudisha uoto wa asili ulioharibiwa katika maeneo husika na watoto wa kike 3140  kutoka familia za walengwa wenye umri wa miaka 11  walipatiwa taulo za kike za kisasa na vifaa vya usafi na baadhi ya Kaya zimeboresha makazi, kujishughulisha na kilimo ,  kufuga mifugo midogo midogo  kama kuku, bata, kondoo na mbuzi, kadhalika kuanza biashara ndogondogo.

Tangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI October 11, 2021
  • ZABUNI January 31, 2017
  • SOMA KATIBA ILIYOPENDEKEZWA March 24, 2017
  • UTARATIBU WA UHAMISHO KWA WATUMISHI WA UMMA March 24, 2017
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • Mfumo wa TAUSI watambulishwa kwa wafanyabiashara

    March 23, 2023
  • Shule ya Msingi Tambukareli yaanza kutumika rasmii

    March 06, 2023
  • Shule ya Msingi Tambykareli yaanza kutumika rasmi

    March 06, 2023
  • DC SHAKA ASISITIZA UONGOZI WA PAMOJA

    March 01, 2023
  • Angalia zote

Video

HIFADHII YA WANYAMA MIKUMI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • MFUMO WA PLANREP

Kurasa za Mfanano

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • NECTA
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737-847-880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa