• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

Kilosa yatarajiwa kuongeza kiwango cha watalii baada ya mbuga ya Mikumi kuboreshwa- Mh. Londo

Posted on: January 28th, 2022

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imefanikisha upatikanaji wa dola milioni 69 ambazo miongoni mwa shughuli zitakazofanyika kupitia fedha hizo ni kuboresha mbuga ya Mikumi ambapo kutakuwepo kiwanja cha ndege cha kisasa kitakachowezesha ongezeko watalii na pato kwa mbuga ya Mikumi na vijiji  jirani.

Hayo yamebainishwa na Mbunge wa Jimbo la Mikumi Mh. Dennis Londo wakati wa zoezi la uhamasishaji chanjo ya Uviko -19 na ushiriki wa sensa ambapo amesema idadi ya watalii itaongezeka kwa kasi ambapo wananchi watashiriki kikamilifu katika shughuli za kitalii kwa vijana kufadhiliwa kimasomo katika kozi zinazohusiana na shughuli za kitalii jambo litakalosaidia kukuza uchumi kiujumla.

Pamoja na hayo ameishukuru Serikali na Chama Cha Mapinduzi chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuiwezesha jimbo la Mikumi kwa ujenzi wa shule mpya ya sekondari na msingi, nyumba ya watumishi wa afya na mashine ya mionzi itakayowekwa katika kituo cha afya Mikumi huku akitoa rai kwa wananchi kujitokeza katika zoezi la sensa ya watu na makazi inayotarajiwa kufanyika mwezi Agosti mwaka huu ambapo kupitia zoezi hilo itasaidia Serikali kupata idadi sahihi ya wananchi na kupanga mipango ya kuwahudumia wananchi kwa  kadri ya idadi yao.

Katika kampeni hiyo ya uhamasishaji Mh Londo, Mkuu wa Wilaya na Katibu wa CCM Wilaya viongozi hao wameshiriki ujenzi wa chumba cha darasa katika kijiji cha Ihombwe ambapo Mkuu wa Wilaya Alhaji Majid Mwanga  ametoa wito kwa wananchi ambao hawajachanja kuchukua hatua kwani yapo baadhi ya maeneo takwimu za uchanjaji haziridhishi kutokana na mwitikio mdogo wa wananchi ambapo amewataka wananchi kutambua kuwa chanjo inasaidia kujikinga na Uviko-19 na ni salama na haina madhara yoyote, huku Katibu wa CCM Wilaya Comrade Shaban Mdoe akiwashauri ambao hawajachanja kuchukua hatua madhubuti za kuchanja kwa ajili ya musatakabali wa afya zao na kuwataka kuachana na propaganda ambazo hazina ukweli wowote kuhusu chanjo sambamba na kutoa rai kwa viongozi wa vijiji kuunga mkono juhudi za wenyeviti wa vitongoji pindi wanapoanzisha shughuli za maendeleo katika maeneo yao..

Nao viongozi wa dini wametoa rai kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kupata chanjo kwani ni salama na haina madhara yoyote huku wakibainisha kuwa lengo la chanjo ni kuhakikisha watanzania wanakuwa na afya njema ambapo pia wamesisitiza ushiriki wa zoezi la sense ya watu na makazi pindi litakapoanza kwani sensa ni muhimu kwa ajili ya maandalizi ya bajeti na utoaji huduma katika jamii na maendeleo ya nchi kiujumla..

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa