• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

KILOSA YATUMIA KILIMO CHA KARAFUU KUBORESHA LISHE MASHULENI

Posted on: April 24th, 2025

Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa imepokea miche 16,000 ya karafuu kutoka katika Taasisi ya TAHA na kuisambaza kwa baadhi ya shule ambapo shule hizo zitaanza kuvuna mazao hayo na kupata fedha zitakazosaidia kununua chakula kwa lengo la  kuhakikisha wanafunzi wote wanapata chakula cha mchana mashuleni.

Hayo yameelezwa Aprili 24, 2025 na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Ndg. Elia Shemtoi katika kikao cha kujadili afua za lishe kwa kipindi cha robo ya tatu kwa mwaka wa fedha  2024/2025 kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa ambapo alieleza kuwa baada ya miaka minne, shule hizo zitaanza kuvuna mazao hayo ya kimkakati.


Pia Kikao hicho kimepitia mpango na matumizi ya fedha za lishe ambapo Ndg. Shemtoi alisisitiza kuwa hatua hii inalenga kuhakikisha kuwa wanafunzi wanapata lishe bora na kutokomeza udumavu wa akili shuleni  jambo ambalo ni muhimu kwa maendeleo yao ya kielimu na afya kwa ujumla.


Aidha, aliwasihi wazazi kutambua umuhimu wa lishe kwa watoto na kuchangia chakula shuleni huku akisisitiza kuwa ushirikiano wa wazazi ni muhimu katika kuhakikisha kuwa watoto wanapata mlo kamili shuleni, ambao unachangia katika ukuaji na maendeleo yao pia akiwahimiza walimu na viongozi wa shule kutumia maeneo ya kilimo yaliyopo shuleni kulima mazao ya chakula ili kuongeza upatikanaji wa lishe shuleni.

Akizungumza katika kikao hicho, Mratibu wa Lishe wa Wilaya ya Kilosa, Ndg. Elisha Kingu, alieleza kuwa licha ya asilimia 87.6 ya shule wilayani humo kutoa chakula shuleni, bado kuna idadi kubwa ya wanafunzi wanaokosa mlo wa mchana na kwamba hali hii inatokana na changamoto mbalimbali, ikiwemo uelewa mdogo wa wazazi kuhusu umuhimu wa kuchangia chakula shuleni.

Kwa upande wao, Maafisa Elimu wa Msingi na Sekondari walikiri kuwepo kwa changamoto hiyo, wakieleza kuwa baadhi ya wazazi hawajitokezi kuchangia chakula kwa watoto wao. Hata hivyo, waliongeza kuwa baada ya msimu wa mavuno, wanatarajia idadi ya watoto wanaopata chakula shuleni itaongezeka, kutokana na wazazi kuwa na uwezo zaidi wa kuchangia.

Naye Mkuu wa Kitengo cha Fedha na Uhasibu Dismasi Mgao alihimiza shule zinazomiliki maeneo ya kilimo kutumia fursa hiyo kulima mazao mbalimbali na kupanda bustani za mboga mboga ambapo alieleza kuwa hatua hiyo itasaidia kuongeza upatikanaji wa chakula shuleni na kupunguza utegemezi kwa michango ya wazazi pekee.


Kikao hicho kilihitimishwa kwa kuwataka wadau na jamii kusimamia na kuendelea kushirikiana katika kuhakikisha kuwa watoto wanapata lishe bora shuleni, ili kuboresha afya na maendeleo yao ya kielimu.




Tangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA WAHE. MADIWANI May 22, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • WAUGUZI WATAKIWA KUWA WAADILIFU MAHALI PA KAZI

    May 30, 2025
  • WAHE. MADIWANI WAISHUKURU SERIKALI YA AWAMU YA SITA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    May 30, 2025
  • KILOSA YAJIPANGA KUTATUA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI

    May 28, 2025
  • VITENGO VYA HABARI SERIKALINI VIIMARISHWE KWA KUFANYA MAWASILIANO YA KIMKAKATI

    May 24, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa