• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

KUKATA MITI HOVYO KUNAANGAMIZA MISITU

Posted on: December 19th, 2018

Imeelezwa kuwa misitu mingi inaangamia ama kuteketea kutokana na umaskini ambapo hakuna namna misitu inaweza ikapona kutokana na kukithiri kwa ukataji miti kwa ajili ya mkaa ambao mahitaji yake ni makubwa katika maeneo mbalimbali hasa katika jiji la Dar es salaam ambapo watu wamekuwa wakikata miti bila kufuata utaratibu na kwamba licha ya mahitaji hayo makubwa ya mkaa hakuna sera ya Taifa inayotoa maelekezo  ya namna gani mahitaji haya yaweze kufikiwa kwa njia endelevu bila kuathiri ikolojia na uchumi.

Hayo yamebainishwa na Afisa Maliasili Mkoa wa Morogoro Joseph Chuwa wakati wakurugenzi toka TAMISEMI walipotembelea wilayani Kilosa ikiwa ni ziara ya  siku tatu katika vijiji vya Ulaya Mbuyuni, Ihombwe na Kitunduweta ili kujifunza nini kinachofanyika kupitia mradi wa mkaa endelevu kwa kushirikiana na TFS pamoja na Halmashauri ya wilaya ya Kilosa ambapo amesema mradi wa mkaa endelevu unaofanya kazi katika vijiji 20 wilayani Kilosa lengo likiwa kuhakikisha wananchi wanachoma mkaa katika njia endelevu kwani mkaa unatakiwa uzalishwe katika njia endelevu jambo litakalosaidia utunzaji wa misitu.

Naye Mkurugenzi Msaidizi wa Shirika la Hifadhi ya Misitu ya Asili Tanzania Emmanuel Lyimo amesema kuwa kwa tafiti zilizofanywa na Wizara ya Maliasili Tanzania inapoteza kiasi cha misitu hekta zisizopungua laki nne kwa mwaka visababishi vikiwa ni kipato ambacho mwanadamu kubadilisha matumizi kutoka katika hali ya misitu na kuwa shamba kwa ajili ya kilimo pamoja na ufyekaji wa misitu kwa ajili ya mkaa ambapo ameshauri ili kukabiliana na hali hiyo ni vema serikali ikawa na misitu yake ya uvunaji na vijiji vikawa na misitu yake ya uvunaji ambayo itasimamiwa na kuiendeleza.

Aidha Lyimo ametoa ombi kwa TAMISEMI ijifunze muundo huo uliyotambulishwa na TFCG ili kuona namna unavyofanya kazi na kuusambaza nchi nzima kwani kupitia muundo huo utasaidia vijiji kutenga maeneo na kunufaika na misitu kwa kutumia rasilimali za hapa hapa nchini ambapo vijiji vitaweza kunufaika na kipato kinachotokana na misitu ili jamii iweze kunufaika ikiwemo usimamizi wa fedha kwani vijiji vingi vilivyopo katika mradi hali ya misitu ni nzuri kuliko ya vijiji ambavyo haviko kwenye mradi.

Naye Mkurugenzi wa Serikali za mitaa Dkt. Charles E. Mhina kwa niaba ya wakurugenzi wenzake toka TAMISEMI  amesema kuwa idara yake inapotembelea Kilosa imelenga kuangalia namna Wilaya inavyotekeleza mradi, namna inavyotunza misitu kwa kuwa na unyevunyevu mzuri lakini pia ziara yao imekusudia kupokea changamoto na kuziwasilisha serikali sambamba na kuishauri juu ya changamoto mbalimbali zinazoikumbuka wilaya lakini pia namna ambavyo Halmashauri ingependa kupokea maelekezo ya kisera.

Sambamba na hayo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Mh. Hassan S. Mkopi amesema kuwa  mradi wa mkaa endelevu umekuwa wa manufaa kwani umekuwa ni shirikishi na vijiji vyenye mradi wananchi wamenufaika kwa kupata ofisi za vijiji, Halmashauri imekuwa ikipata mapato kupitia misitu, ujenzi wa madarasa, wananchi wamefanikiwa kulipia CHF, kipato kimeongezeka kwa wananchi, kuna ongezeko la kipato ka ajili ya miradi ya maendeleo ya jamii na Halmashauri na kuboresha afya ya jamii, kuboresha, pamoja na hayo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Asajile Lucas Mambambale amesema kuwa Halmashauri haiwanyang’anyi wananchi chochote wanaojihusisha na mradi wa mkaa endelevu bali inatekeleza sheria za nchi kwa kutoa utaratibu ambao ni sahihi kwa wananchi kuufuata.

  

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa