• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mipango
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mifungo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

KUPINGA UKATILI NI SUALA LA KILA MTU

Posted on: September 20th, 2018

Imeelezwa kuwa mfumo dume, mila na desturi kandamizi, ukeketaji, kuvunjika kwa baadhi ya mila zilizokuwa zinasaidia ulinzi kwa watoto, matumizi ya madawa ya kulevya na pombe, umasikini ni miongoni mwa mambo yanayosababisha ukatili miongoni mwa jamii.

Hayo yamebainishwa na Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya ya Kilosa Tumaini Geugeu wakati wa kikao cha wadau wa masuala ya watoto ambapo amesema kuwa suala la ukatili linamgusa kila mtu, hivyo jamii kiujumla inapaswa kupinga ukatili ili jamii iweze kukaa salama.

Akieleza zaidi kuhusu ukatili Guegeu amesema jamii itambue kuwa ukatili uko wa aina nne ambapo aina ya kwanza ya ukatili ni ukatili wa kingono ambapo baadhi ya familia baba, mama na watoto hulala chumba kimoja huku watoto wakishuhudia matendo yote yanayoendelea jambo ambalo huzaa ukatili kwa watoto na kusababisha mimba za utotoni, ukatili wa aina ya pili ni ukatili wa kimwili kama vile vipigo, ukatili wa aina ya tatu ni ukatili wa kihisia  ikiwemo maneno ya kuumiza na kudhalilishwa na mwisho ni ukatili wa kiuchumi ikiwemo kutelekezwa na kunyimwa fursa za kiuchumi.

Chanzo kikubwa cha ukatili katika jamii kwa asilimia kubwa huchangiwa na malezi yasiyofaa kwa watoto ambapo hupelekea watoto kadri wanavyokuwa kiumri hujikuta katika tabia zisizofaa ambazo huzaa matendo ya kikatili kama vile ubakaji, vipigo, kunyimwa haki ya kujitetea na kueleza ukweli dhidi ya vitendo viovu ambavyo wazazi ama ndugu huwafanyia watoto, wanawake na hata wanaume kwani ukatili sio kwa wanawake na watoto tu bali hata wanaume.

Jamii inapaswa kufahamu kuwa madhara ya ukatili ni makubwa ikiwemo ongezeko la watoto wa mitaani, ongezeko la wagonjwa waliotelekezwa hasa wazee, migogoro ya ndoa na talaka, maambukizi ya magonjwa ya zinaa, visasi, vifo, ndoa za utotoni, mimba za utotoni pamoja na mendeleo duni ya kiuchumi.

Aidha wadau walioshiriki kikao hicho kwa kushirikiana na Afisa Ustawi wa Jamii wametoa wito kwa wazazi na jamii nzima kutoa ushirikiano katika kesi mbalimbali zinazojitokeza zinazohusu ukatili kwani imebainika kuwa baadhi ya    wazazi kwa asilimia kubwa wamekuwa chanzo kikubwa cha kuendeleza ukatili kwa kutotoa ushirikiano wa kutosha katika kesi hizo na kusababisha haki kutotendeka kwa mtu aliyefanyiwa ukatili.

Tangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI October 11, 2021
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 KWA SHULE ZA SEKONDARI HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOSA July 14, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI September 16, 2023
  • ZABUNI January 31, 2017
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • KILOSA KUDUMISHA USAFI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    September 20, 2023
  • TIMU YA UKAGUZI MKOA YATEMBELEA MIRADI YA BOOST KILOSA

    September 20, 2023
  • MAPATO YA HALMASHAURI YAONGEZEKA KUTOKA ASILIMIA 94 MPAKA ASILIMIA 98.91

    September 01, 2023
  • Walimu watakiwa kuendelea kuzifahamu huduma za kibenki

    August 29, 2023
  • Angalia zote

Video

HIFADHII YA WANYAMA MIKUMI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • MFUMO WA PLANREP

Kurasa za Mfanano

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • NECTA
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737-847-880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa