• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

KUPINGA UKATILI NI SUALA LA KILA MTU

Posted on: September 20th, 2018

Imeelezwa kuwa mfumo dume, mila na desturi kandamizi, ukeketaji, kuvunjika kwa baadhi ya mila zilizokuwa zinasaidia ulinzi kwa watoto, matumizi ya madawa ya kulevya na pombe, umasikini ni miongoni mwa mambo yanayosababisha ukatili miongoni mwa jamii.

Hayo yamebainishwa na Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya ya Kilosa Tumaini Geugeu wakati wa kikao cha wadau wa masuala ya watoto ambapo amesema kuwa suala la ukatili linamgusa kila mtu, hivyo jamii kiujumla inapaswa kupinga ukatili ili jamii iweze kukaa salama.

Akieleza zaidi kuhusu ukatili Guegeu amesema jamii itambue kuwa ukatili uko wa aina nne ambapo aina ya kwanza ya ukatili ni ukatili wa kingono ambapo baadhi ya familia baba, mama na watoto hulala chumba kimoja huku watoto wakishuhudia matendo yote yanayoendelea jambo ambalo huzaa ukatili kwa watoto na kusababisha mimba za utotoni, ukatili wa aina ya pili ni ukatili wa kimwili kama vile vipigo, ukatili wa aina ya tatu ni ukatili wa kihisia  ikiwemo maneno ya kuumiza na kudhalilishwa na mwisho ni ukatili wa kiuchumi ikiwemo kutelekezwa na kunyimwa fursa za kiuchumi.

Chanzo kikubwa cha ukatili katika jamii kwa asilimia kubwa huchangiwa na malezi yasiyofaa kwa watoto ambapo hupelekea watoto kadri wanavyokuwa kiumri hujikuta katika tabia zisizofaa ambazo huzaa matendo ya kikatili kama vile ubakaji, vipigo, kunyimwa haki ya kujitetea na kueleza ukweli dhidi ya vitendo viovu ambavyo wazazi ama ndugu huwafanyia watoto, wanawake na hata wanaume kwani ukatili sio kwa wanawake na watoto tu bali hata wanaume.

Jamii inapaswa kufahamu kuwa madhara ya ukatili ni makubwa ikiwemo ongezeko la watoto wa mitaani, ongezeko la wagonjwa waliotelekezwa hasa wazee, migogoro ya ndoa na talaka, maambukizi ya magonjwa ya zinaa, visasi, vifo, ndoa za utotoni, mimba za utotoni pamoja na mendeleo duni ya kiuchumi.

Aidha wadau walioshiriki kikao hicho kwa kushirikiana na Afisa Ustawi wa Jamii wametoa wito kwa wazazi na jamii nzima kutoa ushirikiano katika kesi mbalimbali zinazojitokeza zinazohusu ukatili kwani imebainika kuwa baadhi ya    wazazi kwa asilimia kubwa wamekuwa chanzo kikubwa cha kuendeleza ukatili kwa kutotoa ushirikiano wa kutosha katika kesi hizo na kusababisha haki kutotendeka kwa mtu aliyefanyiwa ukatili.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa