• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

KUTOKUWEPO UTAWALA BORA HULETA MIGOGORO - DC

Posted on: March 5th, 2019

Kutokuwepo kwa utawala bora kwa viongozi kuanzia ngazi ya vijiji hadi ngazi ya juu sambamba na kutowajibika inavyostahiki kwa mujibu wa mfumo wa serikali ni miongoni mwa changamoto zilizochangia kuwepo kwa migogoro ya wakulima na wafugaji, migogoro ya ardhi pamoja na umaskini.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi wakati wa kikao chake na wazee maarufu, wafanyabiashara, viongozi wa dini, waheshimiwa madiwani wa kata zote za mjini pamoja na watendaji wa kata lengo likiwa ni kujadili hali ya maendeleo wilayani kilosa.

Mgoyi amesema kuwa miaka michache ilopita hali ya kiwilaya haikuwa sawa kutokana na changamoto tajwa ambazo kwa sasa kwa asilimia kubwa zimepungua ambapo amesema kuwa viongozi walikuwa wakiangalia maslahi binafsi jambo ambalo kwa sasa limeaanza kufanyiwa kazi na hali imeanza kuwa shwari

Aidha mgoyi amewataka washiriki wa kikao hicho kutoa mawazo yao kwa namna gani Kilosa inavyoweza kuwa na maendeleo kwani kwa mazingira yaliyopo mabadiliko yanawezekana kwani viongozi wa dini wapo , wanasiasa vilevile ambao wanaweza kuchangia mabadiliko katika sekta mbalimbali.

Wakitoa michango yao kwa niaba ya wenzao mzee Nchimbi Nackam na mzee Antony Fuime wamesema kuwa chanzo cha migogoro ni ukosefu wa umoja wa kutafuta maendeleo sababu kubwa ikiwa ni ubinafsi  katikati ya watu, wanasiasa kukosa nguvu ya ushawishi katika kushawishi wananchi kuchangia maendeleo badala yake siasa zimekuwa zikichukua nafasi kubwa badala ya maendeleo, sambamba na hayo amewaomba viongozi wa dini kutumia majukwaa yao kuhamasisha waumini wao kutumia vema fursa za maendeleo zinazojitokeza.

Naye mzee Peter Thomas pamoja na mzee Raphael Chayeka wameshauri kuwepo kwa zao la kudumu la kutambulisha zao hilo ambalo litakuwa likilimwa na jamii ya watu wa Kilosa ambalo litalimwa kiasi kikubwa na kutafutiwa soko hasa katika kukuza uchumi wa Kilosa, Halmashauri itunge sheria ndogo itakayowalazimisha wazazi kuchangia chakula kwa ajili ya watoto, lakini kuwe na suala la uwajibikaji kwa watumishi ambapo kila mtu awajibike kwa ngazi yake .

Aidha wazee hao wametaka ujenzi wa mji usijengwe kiholela kwani ujenzi holela unasababisha kutokuwa na miundombinu iliyo bora, lakini pia wameomba ufanyike mchakato kwa ajili ya tuta la mto Mkondoa ambalo kwa kiwango kikubwa limekuwa likileta athari kwa wananchi na kurudisha nyuma maendeleo huku upande wa CHF iliyoboresha wamesema baadhi ya dawa muhimu zimekuwa hazipatikani wakati upande wa elimu wameshauri sekta ya elimu iweke namna ya kurudisha elimu kwa watu wazima sambamba na wazazi kuwa kipaumbele katika kuhakikisha watoto wanakwenda shule na kuwa katika mazingira mazuri na salama kwao.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Hassan Mkopi amesema kuwa mawazo, ushauri na changamoto zilizotolewa watazifanyia kazi ambapo pia amewataka washiriki wa kikao hicho kushiriki katika vikao vya vijiji kwenye maeneo wanakotoka kwani maendeleo huanzia ngazi ya chini, hivyo ushiriki wao unaweza kuongeza tija katika kuleta maendeleo lakini pia amemuomba Mkuu wa Wilaya kufikisha salamu za shukrani kwa Mheshimiwa Rais wa awamu ya Tano kwa fedha ambazo Serikali imekuwa ikizitoa kwaajili ya maendeleo ya Wilaya ya Kilosa.

Pamoja na hayo yote Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Rwegerera Katabaro kwa niaba ya ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji ameahidi kuyafanyia kazi yale yote yanayohusu watalaam wa halmashauri kwa kuhakikisha wanafanya majukumu yao kwa mujibu wa taratibu za kazi zinavyowataka na kuwajibika ipasavyo huku Mkuu wa Jeshi la Polisi Kilosa Mayenga Mapalala amesema kwa upande wa Jeshi la Polisi watafanya wajibu wao na kuomba kupatiwa taarifa zote za kiuhalifu ili waweze kuzifanyia kazi kwani ni wajibu wao.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa