• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

LAAC YAITAKA HALMASHAURI KUSIMAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO.

Posted on: March 29th, 2025

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) imeitaka serikali ya Halmashauri ya wilaya ya Kilosa kusimamia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya serikali ikiwa ni pamoja na kusimamia matumizi ya fedha za miradi hiyo lakini pia kuwasimamia wakandarasi wanaotekeleza miradi hiyo ili ikamilike kwa wakati.

Rai hiyo imetolewa Machi 29, 2025 na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Halima Mdee (Mbunge) wakati wa kamati hiyo ilipotembelea miradi miwili ambayo ni ujenzi wa mabweni matatu, madarasa saba na vyoo matundu kumi pamoja na uzio vyenye thamani ya shilingi 612,000,000/= fedha kutoka serikali kuu na shilingi 215,000,000/= kutoka mapato ya ndani katika shule ya Sekondari ya wasichana ya Dakawa lakini pia mradi wa ujenzi wa jengo la Utawala  wenye thamani ya shilingi bilioni 3.6

Akiwasilisha majumuisho ya ziara hiyo, Mhe. Noah Lemburis Mollel (Mbunge) ameitaka Halmashauri kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa kuzingatia ubora na viwango vinavyotakiwa kwa mjibu wa miongozo iliyotolewa na Ofisi ya Rais na Tawala za Mikoa (TAMISEMI).

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI anayeshughulikia Elimu, Atupele Mwambene ameihakikishia kamati ya LAAC kuwa mapungufu yaliyobainishwa kwenye ziara hiyo kuwa yatafanyiwa kazi ikiwa ni pamoja na kutoa ufafanuzi na miongozo kwa watendaji walioko chini ya TAMISEMI wakati wa Utekelezaji wa Miradi hiyo.

Naye Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa ameishukuru kamati hiyo kwa kutembelea miradi hiyo na kutoa maelekezo na maboresho kwenye miradi hiyo na kuahidi kuwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa itashirikiana na Halmashauri katika uboreshaji wa miradi hiyo.

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe. Shaka Hamdu Shaka naye ameihakikishia kamati hiyo kuwa ataendelea kuisimamia Halmashauri katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ili kufikia azma ya serikali ya kuwaletea huduma na maendeleo wananchi.

Akiongea kwa niaba ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa, Mhe. Douglas Mwigumila ambaye ni Diwani wa Kata ya Dumila ameishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kwenye wilaya ya Kilosa.

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa miradi hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Ndg. Beatrice Mwinuka amefafanua kuwa pamoja na mapungufu pamoja na changamoto zilizojitokeza wakati wa utekelezaji wa miradihiyo, Halamshauri imechukua hatua mbalimbali kuhakikisha miradi inakamilika ikiwa ni pamoja na kutenga fedha za mapato ya ndani kwa ajili ya miradi hiyo, kuwateua wasimamizi maalumu wa miradi hiyo lakini pia kuwasimamia wakandarasi wanaojenga miradi hiyo.

Tangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA WAHE. MADIWANI May 22, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • WAUGUZI WATAKIWA KUWA WAADILIFU MAHALI PA KAZI

    May 30, 2025
  • WAHE. MADIWANI WAISHUKURU SERIKALI YA AWAMU YA SITA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    May 30, 2025
  • KILOSA YAJIPANGA KUTATUA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI

    May 28, 2025
  • VITENGO VYA HABARI SERIKALINI VIIMARISHWE KWA KUFANYA MAWASILIANO YA KIMKAKATI

    May 24, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa