• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

LUGOLA ASISITIZA KUDUMISHWA KWA ULINZI NA USALAMA

Posted on: March 10th, 2019

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mh. Kangi Lugola ameziagiza Kamati za Ulinzi na Usalama za Mikoa na Wilaya kuhakikisha zinasimamia uwepo wa ulinzi na usalama na kushughulikia ishara zozote za uvunjifu wa amani ikiwemo maandamano na mikutano ya ndani ya vyama vya kisiasa yenye lengo la kumkashifu Rais ama kuhatarisha usalama wa Mikoa na Wilaya kiujumla.

Kangi ametoa agizo hilo katika mkutano wa hadhara wilayani Kilosa ambapo amesema kuwa licha ya uwepo wa amani na usalama uliopo nchini bado amani na usalama unahitaji kuendelea kudumishwa hivyo ni vema kamati zikadumu katika kudumisha hali ya kiusalama kwa wilaya nzima ya Kilosa.

Akizungumzia juhudi zinazofanywa na Rais wa awamu ya Tano Kangi amesema kuwa Rais amekuwa akifanya mambo mengi yenye tija kwa watanzania waliompa dhamana ya kuongoza nchi ikiwemo kudumisha usalama wa nchi, na kwamba vyombo vya ulinzi na usalama vinafanya kazi kubwa ya kudumisha amani kwani nchi inapokosa amani hakuna jambo lolote la kimaendeleo linaloweza kuendelea.

Kwa upande wa migogoro ya ardhi Kangi amesema mahali popote penye migogoro ya aina hiyo ni dalili za uvunjifu wa amani na kwamba yoyote atakayebainika kusababisha uvunjifu wa amani kamati za ulinzi na usalama zisisite kumchukulia hatua sambamba na kuwachukulia hatua wote wanaohusika kumtukana Rais ama kukashifu viongozi na kwamba mikutano ya kisiasa ilipigwa marufuku na mheshimiwa rais badala yake muda huo utumike kwa ajili ya wananchi kujitafutia maendeleo.

Kangi amewaonya wananchi kutumia kutotumika kuwaficha wahamiaji haramu kwani idara ya uhamiaji itakapowabaini itawashughulikia huku akisisitiza idara ya vitambulisho NIDA kuwapa vitambulisho wale wanaostahili na amewataka wananchi kuepuka vitendo vya wizi hasa katika ujenzi wa reli ya kisasa unaondelea na ametaka wazawa wa Kilosa kupewa kipaumbele katika ajira.

Kwa upande wa Jeshi la Polisi kuwa na nidhamu na kuwahudumia wananchi kwa haki na kuzingatia sheria ambapo amepiga marufuku kukamatwa hovyo kwa boda boda pasipokuzingatia sheria na taratibu za usalama barabarani na kwamba boda boda wapewe elimu badala ya kuwavizia na kuwapiga faini na amesisitiza  pikipiki zinazopaswa kukamatwa na kupelekwa kituo cha polisi ni zile zinazohusika na uhalifu, zinazohusika kwenye ajali na zinazookotwa zisizo na wenyewe.

Aidha kwa upande wa mgogoro wa shamba la Mauzi Estate Kangi amewaagiza wananchi wanaodai kuwa wamepewa eneo hilo ili walilime kuandaa nyaraka zinazoonyesha wamepewa eneo hilo, pili amemtaka mmiliki/mrithi wa shamba hilo Bw. Aris Daimon kuandaa nyaraka zinazoonyesha umiliki wa shamba hilo sambamba na Halmashauri  kuandaa nyaraka zenye maelezo ya shamba hilo na kuziwakilisha kwake ifikapo tarehe 15/03/2019 atakapotembelea tena kata ya Kimamba ili mgogoro huo uweze kufanyiwa kazi kwa kushirikiana na waziri wa Ardhi ili kuepuka uvunjifu wa amani.

           

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa