• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

MAAFISA KILIMO TOENI TAARIFA ZA UTOROSHWAJI MAZAO

Posted on: November 22nd, 2019

Maafisa kilimo wilayani Kilosa wametakiwa kutoa ushirikiano mkubwa wa kutoa taarifa pindi inapojitokeza jaribio la utoroshwaji wa mazao unaofanywa na wanunuzi wa mazao katika kata na vijiji vyao ambao wamekuwa na hulka ya kukwepa kulipa ushuru kwa mazao wanayonunua kwa wakulima kwa lengo la kuyasafirisha bure.

Rai hiyo imetolewa Novemba 21 mwaka huu na Mkuu wa idara ya Kilimo Elina Danstan wakati wa kikao kazi cha maafisa kilimo ngazi ya wilaya, kata na vijiji ambapo licha ya kujadili masuala mbalimbali ya kuboresha kilimo wilayani Kilosa pia amewataka maafisa hao kuhakikisha wanakuwa mstari wa mbele kutoa taarifa za utoroshwaji wa mazao kwani wilaya imekuwa ikipoteza pato kutokana na wanunuzi wachache ambao wamekuwa wakikwepa kulipa ushuru.

Katika kikao hicho mambo mbalimbali yalijadiliwa ikiwemo uwajibikaji wa maafisa ugani kwa kuhakikisha wanakuwa na daftari la orodha ya wakulima, daftrari la huduma za ugani, ujazaji wa opras, ambapo pia wametakiwa kuwa na taarifa za tathmini ya hali ya chakula kwenye maeneo yao lakini pia kutekeleza mpango mkakati wa kilimo msimu wa 2019/2020 kwa kuyatambua na kuyapa kipaumbele mazao ya kipaumbeke ikiwemo pamba, korosho, miwa, mkonge na muhogo sambamba na mazao muhimu ya chakula ikiwemo mahindi, mpunga na muhogo.

Pamoja na hayo wametakiwa kuhakikisha katika maeneo yao wanakuwa na mshamba darasa ili kutoa elimu kwa wakulima wengi, kusimamia matumizi ya kanuni boara za kilimo, kusimamia kalenda ya mazao kwenye skimu za umwagiliaji na usimamizi wa zana bora za kilimo lakni pia wametakiwa kuwa na rejista ya matukio ya migogoro ya wakulima na wafugaji na jinsi ilivyotatuliwa sambamba na kuwa na mfumo mzuri wa kufanya tahmini ya mazao yaliyoharibiwa na mifugo.

Naye Afisa Utumishi na Utawala Wilaya Noel Abel ametoa onyo kwa maafisa hao kuacha mara moja tabia ya kuwatoza wakulima huduma za ugani kwani baadhi ya wakulima wamekuwa wakiwalalamikia maafisa hao kuwatoza huduma ikiwemo kufanyiwa thmini na huduma nyinginezo huku akiwataka  watumishi wote kutambua upandaji wa madaraja/vyeo hutegemea na muundo wa kada husika kwani vipo vigezo vinavyomfanya mtu apande daraja/ cheo ikiwemo ujazaji wa opras, kutimiza miaka mitatu katika cheo husika, kutambua muundo wa cheo unavyoeleza na taratibu zake, pia amewataka maafisa hao kuwepo katika vituo vya kazi kwani baadhi yao wamekuwa watoro kazini ambapo amesema atayebainika kutokuwepo kazini bila ruhusa kwa zaidi ya siku tano atasimamishiwa mshahara.

Sambamba na hayo maafisa hao wameiomba Serikali iitazame sekta ya kilimo kwa jicho la tatu kwa kutoa ruzuku kwa wakulima hasa wakulima wadogo ili kuwainua katika kilimo kwani sekta ya kilimo ndio inayotoa pato kubwa, hivyo inahitaji kuinuliwa zaidi huku wakitoa rai kwa Halmashauri kuwawezesha maafisa kilimo kuunda mashamba darasa katika kila kata huku wakiuomba uongozi wa wilaya kukaa na wadau mbalimbali na kuwapa elimu kuwa wasitumie siasa katika kampeni za kuhamasisha wakulima katika kulima mazao flani flani kwani ahadi mbalimbali zimekuwa zikitolewa pasipo kutekelezwa jambo linalowawia ugumu katika utoaji huduma kwa wakulima.


Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa