• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

MAAFISA UGANI 87 WAPATA NEEMA YA PIKIPIKI ILI KUWAFIKIA WAKULIMA

Posted on: April 6th, 2023

Mkuu wa wilaya ya Kilosa Shaka H. Shaka amewataka maafisa Kilimo kutumia pikipiki walizopewa kwa matumizi sahihi yaliyokusudiwa kwa kuhakikisha kunakuwa na tija kwa wakulima na wilaya kiujumla kwani wilaya ya Kilosa mapato yake kwa asilimia kubwa yanatokana na kilimo.

Shaka ameyasema hayo Aprili 6 wakati wa kukabidhi pikipiki 87 kwa maafisa kilimo zilizotolewa na wizara ya kilimo ambapo amesema kuwa Serikali imetoa kipaumbele katika sekta ya kilimo kwa kuongeze bajeti ya kilimo ili kukidhi mahitaji na changamoto mbalimbali za kilimo kwani kilimo ni biashara lakini pia ni maisha na kwamba ni mategemeo ya Serikali kuona wananchi wananeemeka kupitia kilimo.

Aidha amewataka maafisa hao kutumia vyombo hivyo kwa matumizi sahihi kwa kumuunga mkono Mheshimiwa Rais katika kutimiza maono ya ajenda ya 10/30 ni kwa kutekeleza ajenda hiyo katika kuinua kilimo na kwamba Wilaya Aidha inaamini hakutakuwa na malalamiko toka kwa wananchi juu ya  maafisa hao kutowatembelea kwani tayari wamewezesha usafiri wa kuwafikia wakulima na kuwa msaada kwao.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri Mh.Wilfred Sumari amemshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia mfuko wa Serikali na kutoa pikipiki 87 kwa maafisa kilimo wa Wilala ya Kilosa ambapo ametoa rai pikipiki hizo zitumike kwa matumizi sahihi na kila mmoja atambue na kuheshimu taalama yake na kwamba Halmashauri inategemea tija kutokana na uzalishaji kuongezeka utakaotokana na maafisa hao kuwajibika ipasavyo kwani Wilaya inategemea pato lake kupitia kilimo, huku akiwataka  kuwa sehemu ya kuhakikisha mapato yanayotokana na kilimo yanakusanywa ipasavyo. 

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Bi.Fauzia Nombo amewataka maafisa hao kuzingatia uaminifu na uadilifu katika matumizi ya vyombo vya moto vinavyotolewa na Serikali, ikiwemo kufanya ukaguzi wa mara kwa mara sambamba na kutumia kwa usahihi kwani Halmashauri haitegemei Afisa yoyote kutumia kwa matumizi yasiyo sahihi lakini pia hakutakuwa na malalamiko kwani watapatikana muda wote kutokana na uwepo wa usafiri anategemea utendaji wa kazi utakuwa na tija zaidi kwani watawafikia wakulima na kutoa elimu na msaada kwa mujibu wa majukumu yao, hivyo kupelekea utendaji kazi wa kiwango cha kuridhisha.

Akizungumzia upande wa ugawaji wa pikipiki hizo Mkuu wa Divisheni ya Kilimo na Mifugo Wilaya Dkt. Yuda Mgeni amesema kufuatia upatikanaji wa pikipiki hizo umepelekea maafisa kilimo wote 102 kuwa na pikipiki jambo ambalo litasaidia kuleta mabadiliko kwa wakulima katika uzalishaji kwani watapata huduma kwa wakati,huku Mkuu wa Polisi Wilaya akitoa msisitizo katika matumizi sahihi na sio kwa matumizi binafsi kwani pikipiki hizo ni mali ya Serikali huku akiwataka kuhakikisha wanaziendesha kwa umakini ikiwemo kuvaa kofia ngumu, na kutopakia zaidi ya mtu mmoja.

Jacob Mloka na Khadija Abdala  kwa niaba maafisa Kilimo wenzao wamemshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwatazama kwa jicho la tatu na kuwapatia usafiri ambao utawaongezea ufanisi wa kazi kwani zitawasaidia kuwafikia wakulima kwa wakati na kuleta tija katika sekta ya kilimo kwa Wilaya ya Kilosa.


Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa