• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mipango
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mifungo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

MAARIFA NA JUHUDI VITAONGEZA UZALISHAJI- NAIBU WAZIRI KILIMO

Posted on: October 25th, 2018

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Omari Mgumba amewakumbusha wananchi wote nchini  kuwa kilimo ndio uti wa mgongo wa nchi yetu kwani kupitia kilimo watu wanapata mahitaji mbalilmbali ikiwemo chakula, kipato katika kaya, kuongeza mapato ya wilaya na kuinua uchumi wa nchi kwa ujumla, hivyo ni vema kila mmoja akathamini kazi za wakulima kwani ndio tegemeo la chakula kwa taifa letu la Tanzania.

Hayo yamesemwa Oktoba 24 mwaka huu na Naibu Waziri wa Kilimo wakati wa uzinduzi wa msimu wa kilimo 2018/2019 wilayani Kilosa na kuhamasisha wadau wote katika sekta ya kilimo kufanya kazi kwa juhudi kubwa na maarifa katika kuongeza uzalishaji  na tija kupitia mnyororo wa thamani kwa kila zao na kuinua kiwango cha ushirikiano kwa hali na mali ili kuinua sekta ya kilimo itakayowezesha  wananchi walio wengi kupata kipato na kutoa mchango kwa taifa kuelekea uchumi wa kati ifikapo 2025.

‘‘Serikali ya awamu ya tano imedhamiria kwa dhati kuboresha sekta ya kilimo na miundombinu  ya barabara na reli ya kisasa ambavyo vitasaidia usafirishaji wa mazao na bidhaa hivyo ni rai yangu  kwenu kuchangamkia fursa hii kwa kuzalisha  mazao ya kilimo kwa wingi pamoja na uwekezaji katika viwanda vya kuchakata mazao ili kuongeza thamani’’. Ameongeza Mgumba

Kaulimbiu ya msimu huu ni kanuni bora za kilimo ndio mkombozi wa mkulima tuzifuate, kwa kaulimbiu hii ni matarajio yangu mtautambua mpango mkakati wa kilimo wa wilaya kasha mtautekeleza kwa kuufanyia kazi ili kuboresha kipato cha kaya, jamii na taifa kwa ujumla kwani wilaya hii ina rasilimali nyingi sana ambazo zikitumika ipasavyo zitaleta maendeleo makubwa katika wilaya na kuondoa hali ya maisha duni kwa wananchi hususan wakulima wadogo.

Aidha Mgumba ametoa wito kwa wakulima kujituma, kubadilika, kujibidiisha, kupokea na kutumia mbinu bora za kilimo na teknolojia zinazotolewa  na wataalam kwani miongoni mwa changamoto zinazowakabili wakulima ni kutozingatia kanuni bora za kilimo pamoja na  hivyo wakulima hao wanapaswa kuzingatia kilimo bora kutambua na kuthamini mchango mkubwa wa wadau wa kilimo kwa kutekeleza kwa vitendo teknolojia zote zinazofundishwa na wadau ili kuzalisha malighafi zitakazotumika na viwanda  vilivyopo na vitakavyoongezeka.

Aidha niwajuze kuwa ili muweze kunufaika na uwezeshaji wa kupata mitaji ambayo ndiyo changamoto kubwa mnatakiwa  kujiunga na kuimarisha vikundi na vyama vya ushirika vikiwemo vikundi vya uzalishaji, vyama vya ushirika vya mazao, na vyama vya ushirika vya kuweka na kukopa ambavyo vinaweza kuwa mkombozi kwenu kwa katoa mitaji na elimu ya ujasiriamali ambayo itasaidia kuongeza kipato na kujikomboa kiuchumi.

Sambamba na hayo amewapongeza viongozi wa wilaya katika kupunguza migogoro ya wakulima na wafugaji na kusma kuwa migogoro hiyo kwa kiasi kukibwa inapunguza uzalishaji mazao na uchumi hivto ameusisitiza uongozi kushirikiana na kamati za amani ngazi zote kuhakikisha ufumbuzi wa kudumu unakuwepo baina ya wakulima na wafigaji ili kila mmoja ashiriki kikamilifu kwenye uzalishaji.

Tangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI October 11, 2021
  • ZABUNI January 31, 2017
  • SOMA KATIBA ILIYOPENDEKEZWA March 24, 2017
  • UTARATIBU WA UHAMISHO KWA WATUMISHI WA UMMA March 24, 2017
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • Kilosa kufanya sensa ya mifugo

    December 29, 2022
  • Kilosa kunufaika na mradi wa BOOST

    December 24, 2022
  • Kilosa yaendelea kutambua juhudi za Serikali kwa Watumishi wa Umma na Wananchi-DED Kilosa

    December 19, 2022
  • -Serikali haitosita kulinda Rasilimali watu kwa maslahi ya Maendeleo ya Taifa- Mh. Mhagama

    December 20, 2022
  • Angalia zote

Video

HIFADHII YA WANYAMA MIKUMI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • MFUMO WA PLANREP

Kurasa za Mfanano

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • NECTA
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737-847-880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa