• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

Madiwani Kilosa wapata mafunzo ya kuwajengea uwezo

Posted on: December 5th, 2022

Rai imetolewa kwa Waheshimiwa madiwani  wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa kuwa wasimamizi wazuri na kuepusha migogoro katika maeneo yao kwa kuhakikisha kanuni, taratibu na sheria zinafuatwa.

Rai hiyo imetolewa mwishoni mwa wiki na Mkuu wa Idara Utafiti, Ushauri na Mafunzo ya Muda Mfupi toka Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo Dkt. Muhsin Danga wakati wa kufunga mafunzo ya kuwajengea uwezo madiwani yaliyofanyika katika kwa siku tatu katika kata ya Mikumi ambapo amewataka madiwani hao kutoa ushirikiano wa kutosha ili kuifanya Wilaya na halmashauri kiujumla kusonga mbele.

Katika mafunzo hayo madiwani hao wamejifunza mada mbalimbali ikiwemo sheria ya maadili ya viongozi wa Umma, Elimu ya rishwa, Historia na uhalali wa Serikali za Mitaa, Wajibu na majukumu ya diwani, Uendeshaji wa vikao na mikutano, Usimamizi wa watumishi, Usimamizi wa mapato na manunuzi, Uongozi na utawala pamoja na suala zima la mfumo wa fursa na vikwazo.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Mh. Wilfred Sumari amemshukuru Mkurugenzi Mtendaji kwa mafunzo hayo na kusema kuwa mafunzo hayo yamewaongezea uwezo  na kwamba wameona kuthaminiwa mchango wao kwani mafunzo hayo lilikuwa ni hitaji la madiwani ambapo amewataka madiwani hao kuboresha utendaji wao na kufanya kazi kama timu kwa kushirikiana na watendaji katika maeneo yao ili kuijenga nyumba moja ambayo ni Kilosa huku akitaka kuwepo kwa mpango wa ziara ya mafunzo kwa madiwani ili waweze kujifunza zaidi.

Naye Makamu Mwenyekiti Mh. Hassan Mkopi pamoja na Mwenyekiti wa mafunzo hayo Mh. Douglas Mwigumila wameshukuru kwa mafunzo hayo kwani wanaamini yamewapa maarifa katika utendaji wao na shughuli za Serikali kwa kuleta maendeleo kwenye maeneo yao na kwamba kwasasa wana ari mpya ya kutekeleza majukumu yao kwa kuimarika zaidi kiutendaji huku wakiomba mafunzo hayo kuwa endelevu kwa maslahi ya Halmashauri.

Kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa, Mkuu wa Divisheni ya Utumishi Bi. Fauzia Nombo amewashukuru madiwani hao kwa ushirikiano waliouonyesha katika siku zote za mafunzo na kwamba anaamini kupitia elimu waliyopata watakuwa msaada mkubwa katika maeneo yao hususani katika kupunguza migogoro na malalamiko huku akiahidi kutoa ushirikiano katika kuhakikisha changamoto mbalimbali zinatatuliwa husuasani katika suala zima la kiutumishi.


Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa