• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

Madiwani wahamasishwa kutoa elimu kwa wananchi juu ya utunzaji miundombinu ya barabara

Posted on: February 17th, 2022

Wito umetolewa kwa waheshimiwa madiwani kuwa sehemu ya watoa elimu kwa wananchi katika kutunza miundombinu ya barabara katika maeneo yao kwa kuwaelimisha wananchi kutopitisha mifugo kwenye barabara zilizofanyiwa matengenezo, uendelezaji wa makazi bila kufuata sheria ya mipaka ya barabara sambamba na kutotupa taka kwenye mifereji ya maji ya mvua na kusababisha kuziba kwa makalvati.

Wito huo umetolewa na Meneja wa TARURA Wilaya Injinia Harold Sawaki wakati wa kuwasilisha bajeti kwa mwaka wa fedha 2022/2023 ya Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini(TARURA) ambapo amesema mpango wa bajeti umegawanyika katika  makundi manne ikiwemo matengenezo ya barabara, ukarabati wa barabara na madaraja, ukarabati wa barabara na madaraja kwa miradi ya maendeleo kwa fedha za majimbo na bajeti ya fedha za miradi ya maendeleo(fedha za tozo ya mafuta ukarabati wa barabara na madaraja)  ambazo bajeti inayoombwa ni kiasi cha shilingi bilioni 45 huku akisema kuwa bajeti hiyo imezingatia kukamilisha miradi viporo, uimarishaji wa barabara zenye hali nzuri kwa kuzijengea mifereji ya maji na makalvati na vipaumbele vya matengenezo ya barabara vilivyowasisilishwa kutoka kwenye kata.

Akibainisha changamoto zinazoikabili TARURA amesema ni uchache wa watumishi, ufinyu wa bajeti inayotolewa kwa ajili ya matengenezo ya barabara, wakandarasi wazawa kuwa na mitaji midogo na kutokuwa na wataalam walioajiriwa na kampuni husika hivyo kupunguza ufanisi katika utekelezwaji wa kazi za matengenezo ya barabara na madaraja, ukosefu wa maeneo ya kuchimba madini ujenzi kama vile mawe, mchanga na kokoto na uelewa mdogo wa wananchi juu ya utunzaji wa miundombinu ya barabara.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Mh. Wilferd Sumari amewataka waheshiniwa madiwani na watendaji wa kata kuendelea kutoa elimu kwa wananchi juu ya utunzaji wa miundombinu ya barabara kwa kuhakikisha wananchi walioko katika maeneo yao wanatunza miundombinu hiyo badala ya kuwaachia TARURA jukumu hilo peke yao huku Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Kisena Mabuba akisema kuwa tokea kuanzishgwa kwa TARURA kazi nyingi zimekuwa zikifanyika kwa kasi na kwamba ipo kwa mujibu wa sheria hivyo ni vema waheshimiwa madiwani wakaendelea kuwasiliana nao kwa changamoto mbalimbali wanazokutana nazo.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa