• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

MADIWANI WAONYESHA KURIDHISHWA NA UTENDAJI KAZI WA MKURUGENZI KILOSA

Posted on: June 8th, 2020

Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa wameonyesha kuridhishwa na juhudi za dhati ambazo zimekuwa zikionyeshwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Asajile Mwambambale kwa namna ambavyo amekuwa bega kwa bega kwa kushirikiana na madiwani pamoja na timu nzima ya menejimenti katika kuhakikisha rasilimali za Halmashauri zinatumika kadri ipasavyo na kuleta tija kwa wananchi.

Hayo yamebainishwa Juni 8 mwaka huu na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Mh Hassan Mkopi alipokuwa akifungua baraza la madiwani na kusema kuwa kwa nyakati tofauti tofauti Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa imekuwa na wakurugenzi mbalimbali lakini kupitia Mkurugenzi Mwambambale wanayo mambo ya kujivunia katika usimamizi wa miradi mbalimbali ambapo rasilimali zimekuwa zikitumika vizuri na kuleta tija katika miradi ya maendeleo inayoendelea maeneo mbalimbali na kuleta tija kwa wananchi.

Mkopi amesema kuwa kwa kutambua mchango wa Mkurugenzi huyo waheshimiwa madiwani waliazimia kumtunuku cheti cha pongezi ikiwa ni sehemu na ishara ya kutambua mchango wake kwa Wilaya ya Kilosa lakini  pia ametumia fursa hiyo kumshukuru Mheshimiwa Rais wa awamu ya tano kwa namna ambavyo amekuwa akiitazama Wilaya ya Kilosa ambapo kwa nyakati tofauti tofauti amekuwa akitoa fedha za serikali   ambazo zimekuwa msaada mkubwa katika kuendesha miradi mbalimbali katika sekta ya afya, elimu, maji, kilimo na sekta nyinginezo.

Akionyesha shukrani zake baada ya kupokea cheti cha pongezi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilossa Asajile Lucas Mwambambale amesema anawashukuru madiwani hao kwani utendaji wake wa kazi umechangiwa kwa kiasi kikubwa na madiwani ambao ndio wenye dhamana na Halmashauri na kwamba kama Halmashauri ilijiwekea malengo ambayo yamefanyiwa kazi na kupelekea Halmashauri kufika mahali illipofika.

Mwambambale amesema kama Mkurugenzi na timu ya  menejimenti wamekuwa wakipata ushirikiano mkubwa kutoka kwa madiwani ambao wamekuwa chachu ya kufanya vizuri kwa kuhakikisha miradi yote iliyoko katika kata zao inasimamiwa na kufanyika katika ubora stahiki jambo lililosaidia Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa kuwa mfano wa kuigwa ama chuo cha kujifunza kwa wilaya nyingine ambapo asilimia kubwa ya miradi hiyo imekuwa ikifanyika kwa ubora na thamani stahiki

Pamoja na hayo Mwambambale amewatia moyo madiwani hao na kusema kuwa ni maombi yake kuona madiwani hao wakirejea tena madarakani kwa kipindi kingine ili waweze kuliendeleza mbele gurudumu la maendeleo huku akiahidi kuendelea kufanya kazi zake kwa juhudi kwa kuhakikisha usalama wa rasilimali hususani fedha hadi hapo madiwani watakaporejea tena madarakani na kwamba kasi ya miradi ya maendeleo itaendelea kama kawaida na kwamba kazi zitaendelea kufanyika kwa uadilifu mkubwa kwa kuweka alama za maendeleo katika Wilaya ya Kilosa.

Akibainisha baadhi ya alama zilizowekwa kwa ushirikiano wa madiwani hao amesema kupitia fedha kutoka Serikalini na za mapato ya ndani ya Halmashauri imeweza kuweka alama mbalimbali za maendeleo ikiwemo kutekeleza maagizo ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa jengo la upasuaji Magubike ambalo limekamilika na alama nyinginezo ni ujenzi wa wodi mbili za wanawake na wanaume kituo cha afya Mikumi, ujenzi wa kituo cha afya Malolo, ujenzi wa vyumba vya madarasa shule ya msingi Msowero yamekamilika,  ujenzi wa kituo cha afya na miundombinu ya umwagiliaji pamoja na ghala katika kata ya Mvumi na miradi mingineyo ambayo inaendelea ikiwemo ujenzi wa maabara katika shule za sekondari.

Tangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA WAHE. MADIWANI May 22, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • WAUGUZI WATAKIWA KUWA WAADILIFU MAHALI PA KAZI

    May 30, 2025
  • WAHE. MADIWANI WAISHUKURU SERIKALI YA AWAMU YA SITA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    May 30, 2025
  • KILOSA YAJIPANGA KUTATUA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI

    May 28, 2025
  • VITENGO VYA HABARI SERIKALINI VIIMARISHWE KWA KUFANYA MAWASILIANO YA KIMKAKATI

    May 24, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa