• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

MAKAMPUNI YA MAWASILIANO NCHINI YATAKIWA KUKAMILISHA UJENZI WA MINARA YOTE 758 IFIKAPO MEI 12 2025

Posted on: March 14th, 2025

Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe Jerry William Silaa ametoa agizo kwa Makampuni ya Mawasiliano ya Simu Nchini kukamilisha ujenzi wa Minara ya mawasiliano758 inayoendelea kujengwa nchini kote ifikapo Mei 12, 2025.

Mhe Silaa ametoa agizo hilo Mei 14, 2025 wakati alipokuwa katika Ziara ya kikazi ya siku moja ya  kukagua ujenzi wa Mnara wa Mawasiliano uliopo katika kijiji cha Idete, Kata ya Chanzuru Wilayani Kilosa.

 Amesema kuwa kupitia Mradi huo wa ujenzi wa Minara 758, watanzania zaidi ya milioni 8 kutoka Mikoa tofauti tofauti watafikiwa na kunufaika na Mradi huo huku Mkoa wa Morogoro pekee ukiwa na  jumla ya Minara 69 na kwamba  mpaka sasa tayari Minara 24 imekwisha washwa.

Mhe Silaa amesema kuwa Mnara wa Idete ni miongoni mwa Minara hiyo 758 na unajengwa na kampuni ya Airtel Tanzania baada ya kupata ruzuku kutoka Serikalini ambapo unatarajiwa kukamilika tarehe 1 April mwaka huu na kwamba huduma zinazotarajiwa kutolewa ni  2G , 3G, pamoja na 4G hivyo wakazi wa Kijiji hicho na vijiji jirani wanatarajiwa kupata huduma hizo pindi tu Mnara huo utakapokamilika na  kuwashwa.

Kwa upande wake  Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe Shaka Hamdu Shaka ametoa shukrani zake kwa Waziri huyo wa Mawasiliano kwa kutembelea Wilayani Kilosa na kusema kuwa amekuwa Waziri wa kwanza kufanya Ziara katika Kijiji hicho,sambamba na hayo amesema kuwa Ujenzi wa Mnara huo umetoa fursa ya ajira kwa Vijana wa Kijiji hicho jambo ambalo litawasaidia kujikwamua kiuchumi.

Aidha amewataka Wakazi wa Kijiji hicho  kuendelea kuulinda Mradi huo na Miradi mingine ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali ya awamu ya sita chini ya Mhe Rais Daktari Samia Suluhu Hassan ili iweze kuhudumia kizazi cha sasa na kijacho.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) Mhandisi  Peter Mwasyalanda amesema kuwa Wilaya ya Kilosa ina ujenzi wa Minara 18 kati ya hiyo Minara 9 tayari imeshakamilika na kuanza kutumika huku Mnara huo wa Idete unatarajiwa kukamilika aprili 1 mwaka huu.





Tangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA WAHE. MADIWANI May 22, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • WAUGUZI WATAKIWA KUWA WAADILIFU MAHALI PA KAZI

    May 30, 2025
  • WAHE. MADIWANI WAISHUKURU SERIKALI YA AWAMU YA SITA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    May 30, 2025
  • KILOSA YAJIPANGA KUTATUA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI

    May 28, 2025
  • VITENGO VYA HABARI SERIKALINI VIIMARISHWE KWA KUFANYA MAWASILIANO YA KIMKAKATI

    May 24, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa