• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

MAPATO YA HALMASHAURI YAONGEZEKA KUTOKA ASILIMIA 94 MPAKA ASILIMIA 98.91

Posted on: September 1st, 2023

Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa imefanikiwa  kuongeza  ukusanyaji wa mapato kutoka asilimia 94  mpaka kufikia asilimia 98.91 kwa mwaka fedha uliopita  wa 2022/2023, makusanyo hayo yatasaidia katika shughuli mbalimbali za Maendeleo katika wilaya hiyo.

Hayo yamesemwa 31 Agosti, 2023 na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmasahuri ya Wilaya ya Kilosa Ndg Kisena  Mabuba katika Mkutano wa kawaida wa Baraza la madiwani uliofanyika katika ukumbi wa FDC Ilonga.

Mabuba amesema kuwa mafanikio hayo yametokana na ushirikiano mkubwa uliofanyika baina ya wahe. Wabunge, Madiwani, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya na Watendaji wa halmashauri ambao wamekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha kila mmoja anatimiza majukumu yake.

Ameeleza kuwa katika kipindi cha miaka miwili Halmashauri imeweza kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo kujenga shule za Awali, Msingi na Sekondari mpya ili kupunguza mrundikano wa wanafunzi na pia kuwafikia wanafunzi wanaotembea umbali mrefu kufika shuleni sambamba na vituo vya afya katika kata mbalimbali wilayani hapo.

 Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kilosa Mhe. Wilfred Sumari amesema kuwa maendeleo ya wilaya hiyo yametokana na usimamizi mathubutu wa Mkurugenzi mtendaji na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa kwa  kuhakikisha miradi yote inatekelezwa kwa ufanisi na kwa wakati unaotakiwa.

Aidha akizungumzia upande wa utunzaji wa mazingira Mhe Mwenyekiti amesema Halmashauri imejiwekea Mkakati wa kuhakikisha mazingira na vyanzo vya maji vinakuwa salama kwa kusimamia sheria za mazingira ili kutunza vyanzo hivyo.

Awali katika Mkutano huo Diwani wa kata ya Magubike Mhe. Abuu Msofe aliapishwa na Hakimu Mkazi Mfawidhi Mh. Agnes Ringo baada ya kushinda uchaguzi mdogo uliofanyika Julai 13,2023 baada ya diwani aliyekuwa akiongoza kata hiyo kufariki dunia .



Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa