• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

MAPATO YATOKANAYO NA UTALII YAONGEZEKA,TANAPA YAKUSANYA ZAIDI YA BILIONI 410

Posted on: January 25th, 2025

Imeelezwa kuwa Mapato yatokanayo na Sekta ya Utalii yanazidi kuongezeka ambapo kwa kipindi cha  miezi sita Julai hadi Disemba  2024 shirika la Hifadhi za Taifa  Tanzania  TANAPA limekusanya  kiasi cha Shilingi  325,146,978,076.63  sawa na asilimia  75 .5 ya Malengo ya  makusanyo ya mwaka.

Hayo yameelezwa leo Januari 25,2025 na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye  pia Msemaji Mkuu wa Serikali Bw.Gerson Msigwa, wakati akizungumza na waandishi wa habari  kutoka Mikoa ya Morogoro na Dodoma kuhusu utekelezaji wa Serikali katika Hifadhi ya Taifa Mikumi Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro ambapo amesema Serikali imeendelea kuimarisha matumizi ya teknolojia katika kusimamia shughuli za uhifadhi, ukusanyaji wa mapato, utangazaji wa utalii na fursa za uwekezaji ndani na nje ya nchi.

Amesema katika kuhakikisha dhamana hiyo inafikiwa, Serikali kupitia Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) imeendelea kutekeleza mambo mbambali ikiwemo Kuhifadhi wanyamapori, bioanuai na makazi ya wanyama katika Hifadhi za Taifa kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vya baadae.

Msigwa amesema Shirika limeongeza matumizi ya sayansi na teknolojia katika uhifadhi hasa kwa viumbe adimu na vilivyo katika hatari ya kutoweka ili kuhakikisha ulinzi wao umeimarika na idadi inaongezekana na kwamba wameendelea kuboresha mahusiano na wananchi waishio jirani na Hifadhi kupitia mpango wa ujirani mwema kwa kutoa elimu ya uhifadhi, kutatua migogoro ya mipaka na kushirikiana nao katika maendeleo ya Uhifadhi, ujenzi wa miradi mbalimbali na uboreshaji wa huduma za kijamii.

Pia ameeleza kuwa wamefanikiwa kulipa fidia kwa wakazi zaidi ya 3,500 wa kata ya Nyatwali iliyopo Wilaya ya Bunda Mkoa wa Mara ili eneo hilo liwe sehemu ya hifadhi ya Taifa ya Serengeti kutokana na umuhimu wake katika ikolojia ya wanyamapori na shughuli za uhifadhi.

Katika uhifadhi na utalii,Msigwa amesemakuwa  Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya jitihada kubwa za kutangaza utalii na fursa za uwekezaji nchini na kwamba  jitihada hizo zimezaa matunda kwani ameifungua nchi kiutalii na uwekezaji kupitia filamu aliyoiongoza ya “Tanzania: The Royal Tour” na baadae “The Amazing Tanzania” na kusema  amesema filamu hizo zimeleta matokeo chanya katika sekta ya utalii na kuchangia ongezeko kubwa la idadi ya watalii, sambamba na ongezeko la uwekezaji na mapato yatokanayo na utalii.

Pia, kumekuwa na ongezeko la safari za ndege za moja kwa moja kutoka maeneo mbalimbali ya dunia kuja Tanzania kupitia mashirika kama KLM, Qatar Airways, Emirates na Turkish Airlines, Amesema utalii kwenye Hifadhi za Taifa umeendelea kukua pia idadi ya watalii na mapato yameongezeka mwaka hadi mwaka.

Aidha amesema kuwa watalii wameengezeka,Idadi hii imeongezeka ikilinganishwa na watalii milioni 1,618,538 waliotembelea Hifadhi za Taifa mwaka 2022/2023 ambalo ni ongezeko la watalii 244,570 sawa na asilimia 15.1. huku kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025 Shirika lilikadiria kupokea watalii milioni 1,848,759 ambapo kwa kipindi cha miezi sita Julai – Disemba 2024 watalii milioni 1,146,438 walitembelea Hifadhi za Taifa ambayo ni sawa na asilimia 62 ya makadirio ya mwaka.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa