• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

Posted on: April 29th, 2025

Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa imechukua hatua ya kuboresha usimamizi na ufatiliaji wa marejesho ya mikopo inayotolewa kwa vikundi vya wanawake, vijana, na watu wenye ulemavu kwa kununua gari aina ya Land Cruiser Hard Top yenye thamani ya shilingi Milioni 226 fedha kupitia marejesho ya mikopo ya asilimia 10%.

Hatua hiyo inalenga kuhakikisha ufuatiliaji wa karibu na ufanisi katika urejeshaji wa mikopo hiyo, ambayo ni sehemu ya asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri yanayotengwa kwa ajili ya makundi maalum.

Akizungumza kuhusu hatua hiyo, Mkuu wa Divisheni ya Mipango na Uratibu, Wapa Mpwehwe, amesema kuwa kwa mujibu wa sheria ya mikopo, asilimia 15 ya marejesho ya mikopo hutumika kwa ajili ya usimamizi na ufuatiliaji na kwamba badala ya kutumia fedha hizo kwa posho, halmashauri imeamua kununua gari hilo ili kuongeza ufanisi katika shughuli za usimamizi wa mikopo.

Mpwehwe ametoa wito kwa watendaji wa halmashauri kuhakikisha gari hilo linatunzwa vizuri na kutumika kwa malengo yaliyokusudiwa,huku akiwataka wanufaika wa mikopo hiyo kurejesha kwa wakati ili fedha hizo ziweze kuwasaidia watu wengine katika jamii.

Halmashauri ya Kilosa imekuwa ikitekeleza mikakati mbalimbali ya kuhakikisha mikopo inayotolewa kwa vikundi vya wanawake, vijana, na watu wenye ulemavu inarejeshwa kwa wakati na kutumika kwa malengo yaliyokusudiwa na kwamba hatua ya kununua gari kwa ajili ya usimamizi wa mikopo ni sehemu ya mikakati hiyo ya kuhakikisha ufanisi na uwajibikaji katika utoaji na urejeshaji wa mikopo.

Kwa hatua hyo, Halmashauri ya Kilosa inaonyesha dhamira ya dhati ya kuimarisha mifumo ya usimamizi wa mikopo na kuhakikisha kuwa rasilimali zinazotolewa zinatumika kwa manufaa ya jamii nzima, hasa makundi maalum yanayolengwa na mikopo hiyo.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MRADI WA SHULE YA SEKONDARI MASANZE

    May 20, 2025
  • WATENDAJI NGAZI YA HALMASHAURI WATAKIWA KUWA WAADILIFU

    May 14, 2025
  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa