• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

MATABIBU WA AFYA YA KINYWA WASISITIZA KUTOA ELIMU YA AFYA - DC

Posted on: March 20th, 2019

Machi 20 mwaka huu katika Maadhimisho ya Siku ya Afya ya Kinywa na Meno Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi amewataka matabibu wa afya ya kinywa na meno kupanua afua za kitabibu kulingana na miongozo mbalimbali ya huduma za afya ya kinywa na meno ikiwemo kuwa na ratiba za kutembelea shule za msingi na sekondari kwa lengo la kutoa elimu, ushauri, uchunguzi na matibabu kwa wale watakaobainishwa kuwa na matatizo.

Mgoyi amesema kuwa pamoja na kupanua afua hizo wanatakiwa kuwawezesha kwa kuwajengea uwezo watumishi katika vituo vya afya na wale wanaotoa huduma za afya majumbani pamoja na kuwezesha utoaji wa huduma ya mkoba ya afya ya kinywa na meno ili kuongeza upatikanaji wa huduma kwa wananchi walio mbali na vituo vya kutolea huduma za kinywa na meno.

Akiongea na wananchi waliofika kufanya uchunguzi wa afya ya kinywa na meno Mgoyi amesema kuwa serikali inatambua upungufu mkubwa wa watoa huduma wakiwemo madaktari wa kinywa na meno ambapo Serikali ya awamu ya Tano inaendelea kupambana na kutatua changamoto za watoa huduma za afya ya kinywa na meno lengo ikiwa kurahisisha upatikanaji wa huduma hizo.

Aidha amewataka wananchi kufahamu kuwa uchunguzi wa afya ya kinywa na meno ni muhimu hivyo ni vyema jamii ikahamasi ka na kuwa na hulka ya kwenda hospitali kufanya uchunguzi wa kinywa na meno ili kujihakikishia usalama wa kinywa na meno.

Naye daktari wa Afya ya Kinywa na Meno Mkoa wa Morogoro Dkt Samson Tarimo amesema kuwa kaulimbiu katika maadhimisho hayo ni Sema aaah, chukua hatua zinazingatia katika Afya ya Kinywa na Meno na kwamba lengo la maadhimisho hayo ni kujenga uelewa na kutoa matibabu kwa matatizo ya afya na kinywa na kwamba katika maadhimisho hayo wamefanikiwa kutoa huduma katika shule za msingi Kilosa Town, Mazinyugu na Kichangani sambamba na kwa wananchi ambapo matatizo yaliyobainika ni kuoza na kutoka kwa meno, fizi na mpangilio mbaya wa meno.

Sambamba na hayo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Asajile Lucas Mwambambale amewataka matabibu wa afya kuwa na mpango kazi wa namna ya kutoa huduma kupitia fursa za mikutano mbalimbali ya vijiji ili kutoa elimu  na huduma  ya afya ya kinywa na meno lakini pia amewashukuru wadau mbalimbali na hasa madaktari waliotoa huduma za afya ya kinywa na meno na amewataka kuendelea kutoa huduma kwa kuweka mbele zaidi taaluma yao.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa