• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

MBINU SHIRIKISHI YA UONGOZI YAFANIKISHA KILOSA KUPUNGUZA MIGOGORO KWA ASILIMIA KUBWA-

Posted on: September 18th, 2020

Kupitia ushirikiano ambao umekuwa ukionyeshwa na viongozi mbalimbali wa Wilaya ya Kilosa umekuwa chachu kubwa ya kupunguza migogoro mbalimbali ambayo ilikuwa ikiikabili katika maeneo mbalimbali ikiwemo migogoro ya ardhi, migogoro ya wakulima na wafugaji iliyokuwa ikileta athari mbalimbali katika maisha ikiwemo vifo.

Hayo yamebainishwa Septemba 17 mwaka huu na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi wakati akifungua kikao maalum kilichokuwa kikijadili mpango wa ujenzi wa shule ya sekondari ya bweni kwa ajili ya watoto wa kike akiwa kama mgeni rasmi ambapo amesema kuwa awali kulikuwa na kesi 1580  zilizotokana na migogoro ardhi  na kuleta athari mbalimbali ikiwemo kutokuwepo kwa amani, kutovuna mazao kwa wakati kwa wakulima kuvuna mazao yasiyokomaa na kusababisha mazao kuwa na sumu kuvu ambapo kwa sasa migororo hiyo  imepungua kwa kiasi kikubwa na kufikia kesi 25 hadi kufikia mwezi Machi jambo ambalo ni la kujivunia na sehemu ya mafanikio.

Mgoyi amesema licha ya mafanikio hayo bado wanaendelea kukabiliana na changamoto mbalimbali ikiwemo kukabiliana na baadhi ya wafugaji wanaoendelea kuwaonea wakulima lakini pia wakulima  au madalali wanaoendelea kujinufaisha kwa njia za ulaghai kwa kudai fidia na kujipatia kipato kinyume cha sheria huku akisema upande wa migogoro ya ardhi Serikali ya awamu ya tano imeendelea kufuta mashamba ambayo yamekuwa hayaendelezwi.

Aidha amesema Wilaya ya kilosa inahitaji mwarobaini wa kutibu migogoro ya ardhi ambapo wilaya inahitaji kuwa na mpango bora wa matumizi ya ardhi  mpango ambao anaamini utakuwa ndio suluhisho la migogoro ya ardhi na kwamba anaamini wananchi wataichagua tena Serikali ya awamu ya tano chini ya Mheshimiwa Rais Dkt. John Magufuli ili itakaporudi madarakani kwa kipindi kingine iweze kukamilisha deni hilo kwa wananchi.

Pamoja na hayo amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Asajile Mwambambale kwa juhudi alizozionyesha hususani katika kusimamia na kuhakikisha fedha za ndani zinazokusanywa na Halmashauri kwa asilimia kubwa zinatumika kufanya shughuli za maendeleo ikiwemo ujenzi wa vituo mbalimbali vya afya, ujenzi wa mabweni shule ya sekondari Kimamba, mradi wa maji Ruaha, ujenzi wa jengo la upasuaji Magubike, ujenzi wa madarasa sambamba na ujenzi wa vibanda eneo feri hivyo ni mafaniko makubwa kuona fedha za umma zinatumika ipasavyo.

Pamoja na hayo amesisitiza licha ya kufanikisha mambo mbalimbali lipo jukumu kwa viongozi kwa pamoja kujenga msingi mzuri kwa watoto kwa kuwapatia elimu iliyo bora kwa kuwa na rasilimali watu na majengo pamoja na kuwa na usimamizi mzuri kwa kuhakikisha watoto wanapata elimu bora yenye kuleta tija kwa kuwa na matokeo mazuri katika sekta ya elimu ambapo kwa sasa Wilayaya Kilosa imekuwa ikipanda na kuwa na matokeo mazuri.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa