• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

Mh. Mavunde azindua miundombinu ya umwagiliaji mashamba ya ASA Msimba

Posted on: November 4th, 2022

Novemba 4,2022 Naibu Waziri wa Kilimo, Mh.Antony Mavunde  amezindua rasmi ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji katika mashamba ya uzalishaji wa mbegu yaliyo chini ya Wakala Wa Mbegu za Kilimo(ASA) mradi ambao utakaogharimu kiasi cha shilingi bilioni 18 ikiwa ni utekelezaji wa mpango wa Serikali kuzalisha mbegu bora kwa kipindi cha kiangazi ili kuondokana na changamoto ya uhaba wa mbegu na kuongeza upatikanaji  wake unapofika msimu wa kilimoa mabpo uzinduzi huo umefanyika katika shamba la msimba katika kata ya Chanzuru.

‘’Dhamira ya Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan ni kuondoa changamoto zinazomkabili mkulima ikiwemo upatikanaji hafifu wa mbegu bora msimu wa kilimo, kwa kuona hili Serikali imeongeza bajeti katika kilimo ili kuweka mbiundombinu  ya umwagiliaji kwenye mashamba ya mbegu ambayo itapelekea mbegu bora kuzalishwa kabla ya kuanza kwa msimu wa kilimo, ambapo visima vitano virefu vya maji vilivyochimbwa hapa vitasaidia kuzalisha maji yatakayohifadhiwa katika bwawa lenye uwezo wa kuhifadhi maji lita milioni 45’’. Amesema Mh. Mavunde

‘’Huu ni mwanzo wa mabadiliko makubwa yanayokuja katika uzalishaji wa mbegu bora hapa nchini ili tufikie lengo la uzalishaji wa mbegu wa kutosheleza mahitaji ya nchi na kupata ziada ya kuuza nje ya nchi. Hivyo ASA hakikisheni mnaishirikisha sekta binafsi katika uzalishaji wa mbegu bora kwakuwa ili tuweze kufikia malengo lazima tuunganishe nguvu kwa pamoja baina ya serikali na sekta binafsi na kamwe hampaswi kuwa washindani bali mtegemeane kwa manufaa ya nchi’’.

Aidha Mh. Mavunde amemuagiza Mtendaji Mkuu wa ASA, Dkt. Sophia Killenga-Kashenge kuhakikisha mashamba yote ya ASA yanalimwa na kuongeza uzalishaji wa mbegu, badala ya kuyaacha kama mapori kama ilivyo sasa sambamba na  kuwekewa uzio ili kuyalinda na uvamizi kutoka kwa watu mbalimbali ambao wanayaona kama hayatumiki.

Sambamba na hayo amewaomba wadau wote tushirikiane kwa pamoja katika kutekeleza mipango ya serikali kukuza sekta ya kilimo kupitia utekelezaji wa Vipaumbele vya Wizara ya Kilimo kupitia Ajenda 10/30  ambavyo ni kuimarisha utafiti, kuongeza uzalishaji wa mbegu, kuimarisha huduma za ugani, umwagiliaji na kuwezesha upatikanaji wa masoko ya uhakika kwa mazao ya wakulima.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilosa, Alhaj Majid Mwanga ameishukuru Serikali kwa kupeleka mradi huo mkubwa Kilosa na kusisitiza kuwa wataendelea kushirikiana na ASA bega kwa bega ili mradi huo uweze kuleta tija kwa wananchi wa Kilosa na Tanzania kwa ujumla.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa