• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

MHE. LONDO AKABIDHI AMBULANCE KITUO CHA AFYA ULAYA

Posted on: March 5th, 2025

Mbunge wa Jimbo la Mikumi, Mhe. Denis Londo, amekabidhi gari la kubebea wagonjwa mahututi (ambulance) katika Kituo cha Afya cha Ulaya kilichopo Tarafa ya Ulaya wilayani Kilosa, akitoa shukrani kwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuleta msaada huu muhimu kwa wananchi wa jimbo hilo. 

Katika hafla hiyo, Mhe. Londo amesema kuwa gari hilo litakuwa ni msaada mkubwa katika kuboresha huduma za afya kwa wananchi, hasa wakati wa dharura ambapo usafiri wa haraka ni muhimu na kwamba wananchi wa Jimbo la Mikumi wanahitaji huduma bora za afya, na kuleta gari la kubebea wagonjwa ni moja ya jitihada za serikali kuhakikisha kuwa huduma za afya zinawafikia wananchi kwa wakati.


"Gari hili ni mkombozi kwa wananchi wa Ulaya na maeneo mengine jirani na tunamshukuru Rais Samia kwa kutujali na kutuletea huduma hii, ni muhimu sana kutunza gari hii kama mboni ya jicho ili iweze kutumika kwa muda mrefu na kuendelea kutoa huduma kwa wananchi ambapo linakwenda kutatua changamoto kubwa ya usafiri kwa wagonjwa wa dharura” alisema Mhe Londo.

Katika hatua nyingine wakati akizungumza na wananchi, Mhe. Londo amewataka kutosikiliza maneno ya watu wanaoharibu sifa ya serikali huku akiwakumbusha kuwa serikali ya Rais Samia inatekeleza miradi ya maendeleo kwa manufaa ya wananchi, akitaja ujenzi wa barabara ya lami kutoka Mikumi hadi Kilosa na ujenzi wa karavati kubwa la Nyali kama mifano ya juhudi za serikali kuboresha miundombinu ya wilaya hiyo.

"Serikali ya Rais Samia inatekeleza miradi ya maendeleo kwa ufanisi ambapo Ujenzi wa barabara ya lami kutoka Mikumi hadi Kilosa uko mbioni kuanza, na pia ujenzi wa karavati kubwa la Nyali ambao utawezesha usafiri wa haraka zaidi," alisema Mhe. Londo.


Akizungumza kwa niaba ya wananchi Sara Ally ukomelangani na Mussa Ndekelo wamemshukuru mbunge kwa kuwaletea maendeleo katika jimbo lao ambapo walikua na changamoto ya gari kwa muda mrefu na wengine walikua wanafia na kujifungulia njiani  pamoja na kutumia gharama kubwa za kukodi usafiri hivyo wanaipongeza serikali kwa kuwapatia usafiri huo wa haraka.


Awali akizungumza Mkuu wa Divisheni ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe wilaya ya Kilosa Dkt Seleman Kasugulu ameishukuru serikali kwa kutoa gari la kubebea wagonjwa mahututi, akisema kuwa itakuwa msaada mkubwa kwa wananchi wa maeneo ya vijijini ambapo gari hilo litasaidia kwa kiasi kikubwa usafiri wa wagonjwa kutoka vijijini hadi kwenye kituo cha afya na hospitali, jambo ambalo lilikuwa ni changamoto kubwa kwa muda mrefu.

DMO Kasugulu amesema kuwa kwa muda mrefu, wagonjwa walikuwa wanalazimika kusubiri gari kutoka hospitali kuu ya wilaya ya Kilosa, halo iliyosababisha kuchelewa kwa huduma za afya na kusababisha vifo hivyo kupatikana kwake utakuwa msaada katika kupunguza muda wa kusafiri na kuhakikisha wagonjwa wanapata huduma za afya kwa wakati huku  akisisitiza umuhimu wa kutunza gari hilo kwa ustawi wa jamii.

 

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa