• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

MILIONI 547 ZATOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KILOSA

Posted on: January 21st, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe. Shaka Hamdu Shaka amewata wanufaika wa mikopo ya asilimia kumi ya mapato ya ndani kutumia mikopo hiyo kwa ajili ya kutekeleza shughuli mbalimbali  za miradi wanayoifanya ili kujiongezea kipato kwa mtu mmoja mmoja na kuinua uchumi wa Taifa.

Mhe. Shaka ameyasema hayo tarehe 21Janauari, 2025 wakati wa uzinduzi wa utaoaji wa mikopo ya 10% ambapo katika hafla hiyo Mhe. Shaka amekabidhi hundi ya mfano yenye kiasi cha shilingi Milioni 547,000,000 na kusema kuwa fedha hizo zimetolewa ili zikatekeleze shughuli mbalimbali zinazofanywa na vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

Mhe. Shaka ameongeza kuwa mikopo hiyo imetolewa kwa vikundi hivyo ili vikazalishe na kurejesha fedha hizo kwa wakati ili ziweze kuwanufaisha wananchi wengine.

“Mtakapo rejesha kwa wakati ndipo ambapo  fedha hizo zitakwenda kuwanufaisha  watu wengi zaidi na wanufaika wataongezeka siku hadi siku”. Alisema Mhe Shaka

Aidha Mhe Shaka ametoa wito kwa wakazi wa Kilosa kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kushamirisha maendeleo na kutunza amani ya nchi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Ndg. Michael J. Gwimile  amesema lengo la mikopo hiyo ni kusaidia wananchi waweze kufanya shughuli za kiuchumi. Vilevile amewataka wanufaika wa mikopo hiyo kuendeleza tabia nzuri walizokuwa wakizionesha kabla ya kupokea mikopo hiyo.

“Mkawe mfano kwenye kusimamia miradi yenu, kama lengo ambalo mmeliandika kwenye mradi wakati wa kuomba mkopo mkasimame kwenye lengo hilo”. Alisema Gwimile

Pia Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii Ndg. Alto Mbikiye amesema jumla ya fedha kiasi cha shilingi  Milioni 547zimetolewa kwa vikundi 60 ambapo fedha hizo zimegawanyika katika makundi matatu , 4%kwa wanawake,  4% kwa vijana na 2% kwa watu wenye ulemavu.


Naye mmoja wa wanufaika wa mikopo hiyo Ndg.Iman Mtewele  ameishukuru serikali kwa kuwaamini na kuwapatia mikopo hiyo ambayo itakwenda kuwasaidia kutimiza malengo waliojiwekea ili kuimarisha uchumi wao.

Tangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA WAHE. MADIWANI May 22, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • WAUGUZI WATAKIWA KUWA WAADILIFU MAHALI PA KAZI

    May 30, 2025
  • WAHE. MADIWANI WAISHUKURU SERIKALI YA AWAMU YA SITA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    May 30, 2025
  • KILOSA YAJIPANGA KUTATUA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI

    May 28, 2025
  • VITENGO VYA HABARI SERIKALINI VIIMARISHWE KWA KUFANYA MAWASILIANO YA KIMKAKATI

    May 24, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa