• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

MIRADI YA AFYA NA MAJI KATA YA ULAYA YAZINDULIWA NA MWENGE WA UHURU

Posted on: April 18th, 2025

Katika mwendelezo wa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu, Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa, Ndg. Ismail Ally Ussi, amezindua rasmi Mradi wa usambazaji wa maji katika Kata ya Ulaya, Kijiji cha Ulaya Kibaoni, wilayani Kilosa.



Mradi huo unalenga kuboresha upatikanaji wa maji safi na salama kwa wakazi wa eneo hilo, hususan wanawake na watoto ambao wamekuwa wakikumbwa na changamoto ya kutembea umbali mrefu kutafuta maji.

Akizungumza baada ya kukagua na kupokea taarifa ya mradi huo, Ndg. Ussi ameeleza kuridhishwa kwake na utekelezaji wa mradi huo  wenye thamani ya shilingi milioni 177.9 na kumshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwaletea wananchi wa Kilosa Miradi ya maendeleo ambapo amesisitiza umuhimu wa wananchi kuendelea kumuunga mkono Mheshimiwa Rais katika juhudi zake za kuwaletea maendeleo endelevu.

Sambamba na hayo Ndg. Ussi pia ametembelea mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya cha Ulaya Mbuyuni, ambao umegharimu zaidi ya shilingi milioni 510 ambapo amekagua maendeleo ya ujenzi na kuweka jiwe la msingi, akieleza matumaini yake kuwa kituo hicho kitaboresha huduma za afya kwa wakazi wa eneo hilo na maeneo jirani.

Aidha, kiongozi huyo amepokea taarifa kuhusu hali ya malaria, UKIMWI, lishe, na uchangiaji wa damu salama katika kata hiyo na ametoa wito kwa wananchi kuzingatia lishe bora, kupima afya mara kwa mara, na kushiriki kikamilifu katika shughuli za afya ya jamii ili kuboresha ustawi wao.

Wananchi wa Kata ya Ulaya wameeleza furaha yao kwa ujio wa Mwenge wa Uhuru na Miradi hiyo ya maendeleo na kwamba upatikanaji wa maji safi na huduma bora za afya utaboresha maisha yao na kuchangia katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Mwenge wa Uhuru utaendelea na mbio zake katika maeneo mbalimbali ya wilaya ya Kilosa, ukikagua na kuzindua miradi ya maendeleo, kabla ya kuelekea wilaya nyingine. Kaulimbiu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu ni “Jitokeze kushiriki uchaguzi wa mwaka huu 2025 kwa amani na utulivu”.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa