• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

TIMU YA UKAGUZI MKOA YATEMBELEA MIRADI YA BOOST KILOSA

Posted on: September 20th, 2023

Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa imetakiwa kutekeleza na kusimamia vyema shughuli zote za miradi ya BOOST na kuhakikisha inamalizika kwa wakati na kwa kiwango kinachostahili ili kuleta tija kwa wananchi wa eneo husika.

Hayo yamesemwa 19 Septemba, 2023 na Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Mipango na Uratibu Mkoa Bw. Anza- Amen Ndossa wakati akifanya ukaguzi wa miradi ya Boost katika kata za Mtumbatu, Dumila na Msowero ambapo miradi hiyo hipo kwenye hatua ya umaliziaji. 

Bw. Ndossa amesema kuwa ili kufanikisha miradi hiyo Wahandisi wanapaswa kuzingatia maelekezo  wanayopewa kutoka Tamisemi na kufanya kazi kwa weledi mkubwa ikiwemo kutatua changamoto zinazojitokeza ili kukamilisha miradi hiyo kwa wakati kulingana na bajeti iliyopo,sambamba na hayo pia amepongeza hatua ya miradi ilipofikia.

Bw. Ndossa amesisitiza kuwa shule zote zinatakiwa kuboresha miundombinu ya mifumo ya maji ili wanafunzi pamoja na walimu waweze kupata maji safi na salama katika eneo la shule ambapo itasaidia kuepuka magojwa mbalimbali kama vile Kipindupindu , U.T.I  na Corona lakini pia amewataka viongozi wa viijiji pamoja na kamati za shule kutunza miundombinu hiyo.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashuri ya Wilaya ya Kilosa Bi. Zakhia Fandey amesema kuwa atatekeleza na kuyafanyia kazi changamoto zinazojitokeza kwenye miradi hiyo ili iweze kukamilika kwa wakati  na kufikia lengo lililokusudiwa na Serikali.

Timu hiyo ya ukaguzi ya miradi ya maendeleo ya sekretarieti ya Mkoa wa Morogoro ikiongozwa na Katibu Tawala  Msaidizi wamefanya ukaguzi wa miradi ya BOOST katika kata za Dumila, Mtumbatu na Msowero ambapo kiasi cha shilingi Bilioni 1,089,100,000 zimetolewa  kupitia mradi wa BOOST  kwa ajili ya ujenzi wa shule tatu.

Akitoa mchanganuo wa fedha hizo Fandey amesema Kata ya Dumila ilipokea Mil.475,300,000 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 14 vya madarasa elimu msingi, madarasa 2 elimu ya awali, jengo la utawala, matundu 24 ya vyoo na kichomea taka, Kata ya Mtumbatu ilipokea Sh. Mil 306,900,000 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa 7 elimu msingi, madarasa 2 elimu ya awali, matundu ya vyoo16, jengo la utawala na kichomea taka huku Kata ya Msowero ikipokea Sh. Mil.306,900,000 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 7 vya madarasa elimu msingi, madarasa 2 elimu ya awali, jengo la utawala, matundu 16 ya vyoo na kichomea taka.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa