• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

MISAADA YENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI 50 YAKABIDHIWA KWA WAATHIRIKA WA MAFURIKO KILOSA

Posted on: December 13th, 2023

Waathirika wa mafuriko Wilayani Kilosa wamepatiwa msaada wa mahitaji mbalimbali  kama vile chakula, mavazi, malazi na vyombo  venye thamani  Shilingi Milioni 50 ili waweze kujikwamua kimaisha katika kipindi hiki kigumu.


Akikabidhi msaada huo Disemba 12, 2023 mkoani hapo  Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima amesema baada ya kutokea kwa changamoto hiyo wadau mbalimbali kwa kushirikiana na Serikali imechanga fedha na kununua mahitaji mbalimbali ili kuwasaidia waathirika hao.

Mhe. Malima amesema kuwa wananchi 4700 wameathirika na mafuriko hayo huku nyumba 997 zikizingirwa na maji na nyumba 85 zimesombwa na maji kabisa na wananchi kukosa makazi ya kuishi.

Ameongeza kuwa mafuriko hayo yamesababisha uharibifu wa miundo mbinu mbalimbali ikiwemo madaraja manne na Barabara Pamoja na uharibifu wa mashamba ya vyakula na mali nyingine na kusabisha vifo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe. Shaka Hamdu Shaka ameishukuru serikali, kamati ya ulinzi na usalama za mkoa na wilaya  pamoja na wadau mbalimbali  kwa  ushirikiano wao kwa kutoa misaada hiyo kwa wananchi walioathirika na mafuriko.

Pia Mhe. Shaka amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassani kwa kuipatia wilaya ya kilosa shilingi Bilioni 13 kwa ajili ya kuboresha miundo mbinu ambayo imesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza maafa ukilinganisha na kipindi cha awali huku akibainisha kuwa waathirika hao bado wanahitaji misaada hivyo ameomba wadau mbalimbali kujitokeza kutoa msaada kwa waathirika hao.

Akizungumza kwa niaba ya wadau, Meneja wa Bank ya NMB kanda ya kati Bi. Janeth Shango kwa niaba ya Mtendaji Mkuu wa Bank hiyo ametoa pole kwa wananchi walioathirika Wilayani Kilosa ambapo Benki hiyo imetoa shilingi milioni 10.

Bi. Janeth amesema kuwa Benk hiyo ina utaratibu wa kutoa sehemu ya faida wanayoipata kwa wananchi hususani kwa waliopata matatizo mbalimbali ili kuungana na Serikali katika kupunguza changamoto kwa wananchi ikiwemo hili la mafuriko.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa