• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

MKULAZI KUWA MWAROBAINI WA UHABA WA SUKARI NCHINI

Posted on: May 26th, 2020

Naibu Waziri wa Kilimo Mh. Omary Mgumba ameonyeshwa kuridhishwa na kazi ya maandalizi ya uwepo wa kiwanda cha sukari cha Mkulazi II unaondelea katika kata ya Mbigiri ambapo amejionea kazi nzuri ikiwemo uwepo wa mashamba ya miwa, ujenzi wa nyumba za watumishi, jengo la utawala, uwepo wa vifaa pamoja na ukarabati wa barabara ambayo awali ilikuwa haipitiki. 

Mgumba ameonyeshwa kuridhishwa na maendeleo makubwa yaliyofanyika katika kiwanda hicho cha mkulazi II Mei 26 mwaka huu alipokuwa katika ziara yake ya siku moja katika kiwanda hicho ambapo amepongeza kazi kubwa iliyofanyika chini ya Mkulazi pamoja na uongozi wa bodi na kusema kuwa yapo maelekezo yaliyotolewa na Serikali ambayo kwa kiasi kikubwa yametekelezwa lakini pia amepongeza uongozi wa kiwanda hicho kwa kushirikiana na wabia wao ikiwemo NSSF kwa kufanikisha ununuzi na umiliki wa mitambo mbalimbali ambayo itasaidia katika shughuli nzima za uzalishaji sukari kiwandani hapo.

Mgumba ameonyeshwa kuridhishwa na maendeleo makubwa yaliyofanyika katika kiwanda hicho cha mkulazi II Mei 26 mwaka huu alipokuwa katika ziara yake ya siku moja katika kiwanda hicho ambapo amepongeza kazi kubwa iliyofanyika chini ya Mkulazi pamoja na uongozi wa bodi na kusema kuwa yapo maelekezo yaliyotolewa na Serikali ambayo kwa kiasi kikubwa yametekelezwa lakini pia amepongeza uongozi wa kiwanda hicho kwa kushirikiana na wabia wao ikiwemo NSSF kwa kufanikisha ununuzi na umiliki wa mitambo mbalimbali ambayo itasaidia katika shughuli nzima za uzalishaji sukari kiwandani hapo.


Mgumba amesema yapo maendeleo makubwa ambayo yamefanyika ikiwemo kuendelezwa kwa hekta 1300 za shamba lakini pia umefanyika ununuzi wa mitambo itakayotumika kwa ajili ya shughuli za uzalishaji na mashambani lakini pamoja na udhibiti na ujenzi wa daraja pamoja na uboreshaji wa miundombinu ya umwagiliaji ambayo awali miwa ilikuwa ikiathirika kutokana na ukame lakini kwa sasa kutokana na uboreshaji huo wa miundombinu ya umwagiliaji hali itakayosaidia zaidi ya hekta 700 kunufaika na mbiundombinu hiyo huku akibainisha kuwa utendaji wa Serikali si wa maneno bali kwa matendo ambayo yanadhihirika wazi ikiwemo ujenzi wa kiwanda hicho cha sukari.

Pamoja na hayo Mgumba amesema mradi wa huo ni wa manufaa makubwa kwa Serikali  na nchi kiujumla kwani unakwenda kumaliza tatizo la sukari nchini ambako katika kiwando hicho kwa kuanzia utazalisha takribani tani 50,000 za sukari huku upande wa kiwanda kikubwa cha Mkulazi Estate ukizalisha  zaidi ya tani 200,000 na matarajio ni kufika 2020/24 kutakuwa na uwezo wa kuzalisha zaidi ya tani 250,000 na kwamba tatizo la sukari litakuwa limeisha nchini kwani jicho la Serikali lipo katika kiwanda cha Mkulazi ikiwa ni kampuni itakayokuwa na uhakika wa kuzalisha sukari yenye utoshelevu nchini.

Akielezea suala la upatikanaji wa mbegu Mgumba amesema kiwanda hicho kina mtambo wa kuchemshia mbegu na kutoa uhakika wa mbegu zinatakazotolewa na kutumika kiwandani hapo ni za uhakika na kuepusha hasara kwa nchi kwani kupitia mapungufu mbalimbali yaliyojitokeza Serikali imejiwekea mikakati ya uhakika kwa kushirikiana na kiwanda hicho kwa kuhakikisha mbegu zenye kuleta matokea mazuri na zitatumika katika uzalishaji na kwamba taratibu sahihi zinafuatwa katika uzalishaji miwa kiwandani hapo kwa ajili ya mustakabali wa nchi yetu kwani hatua zote zinapofuatwa katika kilimo cha miwa hadi kufika kiwandani inachukua miaka mitatu.


Akitoa rai kwa wananchi Mgumba amewataka wananchi na wakulima kiujumla kutumia fursa ya uwepo wa kiwanda hicho kinachotarajiwa kufungwa mitambo mwaka huu kuwa wakulima wasisite kutumia fursa ya uwepo wa kiwanda hicho kwa kulima miwa kwa kiwango cha kutosha kwani soko lipo na kwamba Serikali inaendelea kuwekeza katika kiwanda hicho kwa kuhakikisha mahitaji yote yanapatikana huku akiendelea kuipongeza NSSF kwa kutenga bajeti kwa ajili ya kuendeleza mradi huo  ambapo pia amewataka wananchi kuachana na suala la upotoshaji kuwa mfuko kwa ajili ya kiwanda hicho unalegalega kuwa habari hizo si za kweli na kwamba mradi huo upo na una faida kubwa ikiwemo soko la uhakika ndani ya nchi , kuongezeka kwa mapato pamoja na ajira kwa vijana na kwamba uhaba wa sukari unakwenda kumalizika kutokana na uwekezaji unaofanywa na Mkulazi.



Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa