• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

MKULAZI SHIRIKISHENI WAKULIMA WA NJE KWA UKARIBU- DC KILOSA

Posted on: December 12th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi ameutaka uongozi wa shamba la miwa la Mkulazi kutambua umuhimu wa wakulima wa nje kwenye shamba hilo kwani uwepo wa wakulima wa nje utasaidia kwa kiasi kikubwa kukua kwa shamba hilo kwani bila wakulima wa nje kiwanda hakiwezi kufanikiwa.

Mgoyi amesema kuwa wakulima wa nje ni wa muhimu licha ya changamoto mbalimbali zilizowahi kutokea kipindi cha nyuma na kwamba hawapaswi kuangalia changamoto hizo kama kikwazo bali wasonge mbele na kuchukua changamoto hizo kama fursa ya kujifunza na kusonga mbele huku ikitambua umuhimu mkubwa wa wakulima wa nje kwa kuhakikisha katika mipango yao wanawahusisha wakulima wa nje.

Awali changamoto  zilizojitokeza katika kilimo hicho ni miwa kupandwa nje ya wakati, uhaba wa  maji, matunzo hafifu ya mashamba , kutokuwa na uongozi thabiti wa Magole joint, elimu ndogo ya kilimo bora cha miwa ikiwemo kukosa usimamizi na kwamba kwa sasa Mkulazi inapaswa kuwatumia ipasavyo wataalam wa kilimo kwa kuhakikisha wanapata huduma stahiki ili kuondokana na umaskini ili tuweze kuelekea uchumi wa kati kwa mafanikio.

Mgoyi amesema kuwa suala la uzalishaji sukari ni la wote hivyo kila mtu aone umuhimu wa kuwa na kiwanda cha sukari, hivyo ameiagiza Halmashauri na wataalam wake kuhakikisha inawasimamia wakulima walime kwa  utaratibu na usimamizi mzuri ambapo mwisho wa mwaka Halmashauri itakuwa na uwezo wa kupata zaidi ya shilingi bilioni moja kutokana na kodi kupitia kilimo cha miwa, hivyo Halmashauri , Mkulazi ambaye ndio msimamizi  mkuu pamoja na wakulima kila mtu atekeleze wajibu wake ili kufikia malengo hayo na kwamba ofisi yake haitasita kumchukulia hatua yoyote atakayesababisha kutofikia malengo.

Akizungumzia suala la mkopo wa 100% amesema haliungi mkono kwani haiwezekani benki kuwakopesha 100% na kitendo hicho jambo lisilowezekana  duniani na ndilo lililosababisha kufika katika changamoto zilizojitokeza kwani kuhitajika kwa mkopo huo kwa 100% kumefanya athari kwa wakulima kwa kujikuta wakisubiri mkopo badala la kujishughulisha hivyo tatizo hilo litafutiwe ufumbuzi na kwamba mkulima anayejiona hawezi ni vema akaacha kujiingiza katika kilimo hicho.

Naye Meneja wa benki ya Azania tawi la Morogoro Liberia Peter amesema kuwa licha ya changamoto zilizojitokeza hapo awali wapo tayari kutoa ushirikianao na ili benki iweze kutoa pesa wakulima wanapaswa kukubaliana na Mkulazi juu ya mbegu watakazotumia, pili watatakiwa kukamilisha ukomo wa madeni wa vyama vya Ushirika -AMCOS, tatu kuwepo na taarifa za mkulima mmoja mmoja na shamba analomiliki likiwa na hati miliki zinazotambuliwa na Halmashauri,  kuwepo na mkataba mkulima baina ya wakulima na Mkulazi na kwamba vitu vyote vikikamilika benki ya Azania itaendelea kutoa mkopo kwa wakulima.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa