• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

MKUU WA WILAYA YA KILOSA AFANYA ZIARA YA KUJITAMBULISHA KATIKA KATA YA MAGUBIKE

Posted on: June 23rd, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Shaka Hamdu Shaka amefanya ziara yake kwa mara ya kwanza katika kata ya Magubike ikiwa ni muendelezo wa kukutana na wananchi wa kata mbalimbali Wilayani hapa kwa kusikiliza kero za Wananchi wa kata hiyo na kusema kuwa watahakikisha wanatekeleza matakwa ya Ilani ya chama kilichopo madarakani, chama cha mapinduzi (CCM).

Mkuu huyo wa Wilaya amefanya Ziara hiyo juni 22 mwaka huu akiambatana na kamati ya Ulinzi na usalama ya Wilaya hiyo, Katibu Tawala Wilaya bi Salome Mkinga, Pamoja na baadhi ya Wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashauri, kwa kusikiza  changamoto mbalimbali zinazowakabili  wananchi wa magubike kwa lengo la kufanyia kazi changamoto hizo.

Mh Shaka  amesema kuwa  Viongozi wa wilaya ya Kilosa wapo kwa ajili ya wananchi wa Magubike na Kilosa kwa ujumla kwa kuwatekelezea mambo mbalimbali ya nayohusu maendeleo na uchumi kwa wananchi hivyo anaomba ushirikiano  kwa viongozi wa wilaya hiyo pamoja na wananchi ili kufanikisha utekelezaji wa ilani ya Chama hicho kilichopo madarakani . 

Aidha baadhi ya  wananchi  wametoa  kero  mbalimbali zinazowakabili ikiwemo uhaba wa maji, ubovu wa barabara ya mwandi-magubike, kukosekana umeme katika baadhi ya vitongoji, migogoro ya mipaka kati ya kijiji cha ibindo na chaumbere,  kukosekana kwa kituo kidogo cha polisi,  uhaba wa vyumba vya madarasa na matundu ya vyoo katika shule ya msingi magubike, uhaba wa chakula na ukosefu wa Zahanati katika kitongoji cha Mwandi.

 Naye Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya  kilosa Dr Yuda Mgeni amesema kuwa wamepokea kero hizo na kuahidi kuzifanyia kazi, ambapo kuhusu uhaba wa chakula amesema kuwa tayari kama Wilaya wameshapitisha timu kwa ajili ya kufanya tathmini ili kubainisha hali ya chakula baada ya kuona mwenendo wa hali ya hewa siyo mzuri na tayari ripoti imekamilika na kuwasilishwa katika mamlaka ya hifadhi ya chakula NRFA hivyo mchakato ukikamilika chakula hicho cha bei nafuu kitaletwa kulingana na mahitaji ya wananchi.

Kwa  upande wake Mkuu wa kituo cha polisi Dumila ASP Emmanuel Mabembere ambaye alimwakilisha Mkuu wa Polisi Wilaya (OCD)ametoa Rai kwa wananchi na madereva wanaotumia vyombo vya moto  hususani bodaboda kufuata na kuheshimu sheria za barabarani  ili kuepuka ajari zisizo za lazima pia amesisitiza  kila mmoja kuwa mlinzi wa mwingine ili kuepuka uhalifu katika maeneo  yao.


 

 

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa