• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

MKUU WA WILAYA YA KILOSA AMEWATAKA WANANCHI KUISHI KWA KUFUATA SHERIA NA UTARATIBU

Posted on: September 23rd, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe. Shaka Hamdu Shaka amekemea vikali vitendo viovu  vinavyofanywa na baadhi ya wafugaji dhidi ya wakulima kwa kujichukulia sheria mkononi bila kufata utaratibu wa kisheria na kusababisha hali ya uvunjifu wa amani katika makazi ya wananchi wilayani hapo.

Mhe. Shaka ameyasema hayo  katika ziara yake ya siku mbili zilizofanyika  tarehe  20 na 21 septemba, 2023  ambapo amesikiliza changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi wa kata ya mikumi kitongoji cha mbegesera sambamba na kata ya Masanze kitongoji cha Dodoma isanga ambapo wananchi  walipata nafasi ya kuzungumza changamoto  zinazowakabili kama vile migogoro ya wafugaji na wakulima.

Katika mikutano hiyo ya hadhara Mhe. Shaka amesema kuwa tayari zipo hatua za awali ambazo zimeshachukuliwa kwa ajili ya kutatua changamoto hizo na bado Serikali inaendelea kuchukua hatua stahiki katika kutatua migogoro ya wafugaji ambayo ni tatizo kubwa katika kata hizo na kuhakikisha wananchi wanaishi kwa utulivu, amani na usalama.

Aidha Mhe. Shaka amesema kuwa hafurahishwi na vitendo hivyo viovu kutoka kwa wafugaji hao ambao wamekuwa tishio kubwa kwa wakulima kwa kuwafanyia kuharibifu wa mazao katika mashamba yao na wakati mwingine kuwajeruhi kwa kutumia silaha za jadi na kusababisha uchumi wao kudidimia.

Sambamba na hayo Mhe. Shaka amewataka wananchi  kuendelea kutoa ushirikiano wao kwa jeshi la polisi ili kutokomeza vitendo hivyo viovu na kuendelea  kuiamini serikali yao ambayo lengo lake ni kuhakikisha ulinzi na usalama ni haki ya kila mwananchi. 

Naye Mkuu wa Divisheni ya Kilimo, Uvuvi na Mifugo Dkt. Yudah Mgeni amesisitiza wananchi  kuishi kwa kuzingatia mpango wa matumizi bora ya ardhi kwani wananchi wote wanategemeana na hakuna aliyebora zaidi ya mwingine.

 Akiongea kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Contantine Nzila amesema kuwa migogoro hiyo inayosababishwa na wafugaji bado ni changamoto katika vitongoji hivyo, kitu ambacho ni tishio kwa usalama wa wakulima pamoja na mali zao hivyo kwa kushirikiana na viongozi wengine na wadau mbalimbali  watahakikisha migogoro hiyo inatatuliwa kwa kufata utaratibu wa kisheria.

 Mbali na migogoro ya wafugaji na wakulima pia wananchi hao walibainisha kero mbali mbali kama vile kuchelewa kufika kwa huduma ya  umeme, ukosefu wa maji pamoja na ubovu wa barabara kutoka miyombo mpaka Dodoma isanga kata masanze ambayo ina umbali wa km.10.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa