• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

MVUMI WAPATA ELIMU YA KUTUMIA FURSA

Posted on: January 31st, 2020

Wakulima wa kata ya Mvumi wametakiwa kutambua kuwa fursa ni uwezekano wa kufanya kitu au jambo halali kwa lengo la kuongeza kipato katika sekta mbalimbali ikiwemo kilimo au biashara ambapo katika kilimo wametakiwa kufanya kilimo biashara kwa kuwa na matokeo chanya ya kitu wanachotaka kukifanya katika mtazamo wa kupata faida.


Hayo yamebainishwa na Anthony Temu Meneja Urasimishaji Rasilimali Ardhi Vijijini toka Ofisi ya Rias MKURABITA ambapo ameseama ni vema kuwa na mtazamo wa kupata faida kabla ya kufanya jambo kwa kuwa na uwezo wa kupanga kabla ya kufanya ambapo amesema kuwa tatizo ni fursa hivyo yanapojitokeza mtu anapaswa kuwaza na kupanga namna ya kulitatua kwa kulenga kupata faida.

Temu amewataka washiriki wa mafunzo hayo kutambua kuwa kila aliyefanikiwa lipo jambo alilofanya hivyo amewataka kuwa na mtizamo  chanya na kuwa na wivu wa maendeleo hivyo ni vema watu wakawa wadadisi wa kutaka kujua mambo na kujifunza kupitia watu wengine ikiwemo kutafuta taarifa mbalimbali.

Temu amesema fursa zinaweza kutambuliwa kwa kupitia ongezeko la watu kwani watu ni soko lakini pia ni uchumi kupitia mahitaji mbalimbali ya jamii ambayo inaongezeka hivyo mtu anaweza kutumia fursa ya ongezeko la watu kutoa huduma kupitia mahitaji yao lakini pia amewataka kutambua kuwa uwepo wa miradi ni sehemu ya fursa kwa kuangalia nini cha kufanya ili kupato  kipato tofauti.

Sambamba na hayo amesisitiza uthubutu wa kutumia fursa husika lakini pia kutumia ukuaji wa uchumi kama fursa kwani  kadri uchumi unavyokuwa ndivyo na mzunguko wa fedha ulivyo hivyo amewataka washiriki hao kujua namna ya kuizuia fedha na kuifanya ikae mikononi mwao kwa kuwa na mtizamo wa kujiwezesha kiuchumi na kuwa wajasiliamali kwa kuangalia namna kujipatia kipato .

Akizungumzia suala la ujasiriamali Temu amesema ujasiriamali ni ule mshawasha wa kupata mali hivyo ili kufanikiwa ni lazima kuwe na ujasiri katika kutafuta mali na kubadili mtazamo kwa kuwa na uwezo wa kutambua kwa haraka changamoto na kuzifikiria na  kuzigeuza fursa kwa kuwa na ubunifu kwani mjasiriamali ni lazima awe tofauti na mwepesi wa kubuni mambo kwa faida.

Aidha amewashauri kabla ya kufanya jambo kutafuta utaalam dhidi ya jambo wanalopanga kulifanya ili kupata elimu juu ya jambo husika ili pindi wanapoamua kufanya jambo wawe na elimu ya jambo husika jambo litakalowasaidia kulifanya kwa ufasaha zaidi.

 

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa