• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

MWANAMKE NI MSINGI WA MAENDELEO

Posted on: March 9th, 2020

Mwanamke ni msingi wa mabadiliko katika familia hivyo anapaswa kushirikishwa katika kufanya maamuzi ambapo wanaume na wanawake wanapaswa kushirikiana katika kazi za Maendeleo ya familia lakini pia ipo haja ya kukumbushana umuhimu wa kizazi cha usawa katika kufikia malengo ya maendeleo endelevu katika ngazi zote za kuamua, kupanga, kutekeleza na kutathmini katika mipango yetu ya kila siku ili kuinua kipato katika familia.

Hayo yamebainishwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Christina Hauli katika maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani ambayo huadhimishwa Machi 8 kila mwaka ambapo Kauli mbiu ya mwaka huu 2020 ni  “Kizazi cha Usawa kwa Maendeleo ya Tanzania ya Sasa na Baadaye”. Kauli mbiu  inayolenga kuelimisha, kuhimiza na kuhamasisha umma kuhusu umuhimu wa usawa wa  kijinsia katika kufikia malengo ya maendeleo endelevu .

Hauli amesema maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ni mojawapo ya mkakati wa Serikali katika kujenga uchumi na Taifa linalojitegemea kuelekea uchumi wa kati, kwa misingi ya utekelezaji wa  Sera ya Maendeleo ya Wanawake na Jinsia (2000), na Dira ya Taifa ya Maendeleo (2025) ni mojawapo ya miongozo ya Serikali unaotoa mwelekeo wa kushughulikia maendeleo ya wanawake kwa kutumia kizazi cha usawa, sera ambayo inatambua umuhimu wa maendeleo ya uchumi kijamii, kisiasa na kiutamaduni kwa wananchi wa jinsi zote.

Aidha amesisitiza viongozi katika ngazi mbalimbali kuwa chachu na wahimizaji wakuu katika utekelezaji wa Seraambao unatilia mkazo uchambuzi wa kijinsia kuwezesha uingizaji wa masuala ya kizazi cha usawa katika mipango, program na miradi ya maendeleo ambapo jamii ikielimika vilivyo, siku ya Wanawake hatutazungumzia matatizo na vikwazo vya kinamama badala yake tutakuwa tukipima maendeleo yaliyofikiwa kwa nguvu zao kupitisha mipango yao.

Hatahivyo Hauli amesema Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa inatambua kikamilifu kwamba wanawake na wanaume wana mchango mkubwa sana katika mipango na miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo ambapo kwa kuamini hivyo wanaume na wanawake wana jukumu na wajibu  katika utekelezaji wa mipango ya maendeleo kwa lengo la kuinua kipato cha kaya na taifa kwa ujumla.

Pamoja na hayo Hauli amesema licha ya jitihada nyingi kufanyika bado kuna vitendo vya unyanyasaji na ukiukwaji wa haki za binadamu na hususani haki za Wanawake ambapo ametaka kutumika kwa vyombo mbalimbali vya msaada ili kupunguza changamoto hizo ikiwemo Dawati la Jinsia kupitia Polisi, wasaidizi wa kisheria Paralegal, TAMWA pamoja na Ofisi za Ustawi wa Jamii.



Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa