• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

NIDHAMU YA FEDHA YAIFANYA KILOSA KUWA NA MIRADI MIZURI YA MAENDELEO

Posted on: June 7th, 2020

Usimamizi mzuri wa matumizi ya fedha za mapato ya ndani pamoja na nidhamu ya matumizi pamoja kupunguza matumizi yasiyo ya lazima  vimekuwa msaada mkubwa kwa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa katika kuhakikisha inakuwa na miradi ya maendeleo ambayo imekuwa ikifanyika katika kata mbalimbali zilizopo wilayani Kilosa na kuifanya wilaya kuwa na hati safi kwa miaka mitano mfululizo ikiwa ni miongoni mwa halmashauri chache zilizofanya vizuri.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Mh Hassan Mkopi wakati wa ziara ya kamati ya fedha, uongozi na mipango iliyokuwa ikitembelea miradi mbalimbali ambapo amesema kuwa kupitia mapato ya ndani sambamba na uwezeshaji wa fedha toka serikalini Halmashauri imefanikiwa kuwa na miradi mbalimbali katika sekta mbalimbali ikiwemo utoaji wa asilimia kumi kwa vijana, wanawake na wenye ulemeavu jambo linalosaidia kwa kiasi kikubwa halmashauri kusonga mbele.


Mkopi amesema anamshukuru sana Mheshimiwa Rais wa awamu ya tano kwa kuitazama Kilosa kwa mapana yake na kuipatia fedha kwa nyakati tofauti tofauti ili kusukuma mbele maendeleo katika wilaya katika sekta ya afya, elimu, kilimo lakini pia amemshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Asajile Mwambmable na timu yake kwa ushirikiano waliouonyesha kwa kuhakikisha fedha zinatengwa kwa ajili ya shughuli za maendeleo ambapo wamekuwa wakishirikiana na waheshimiwa madiwani katika kuhakikisha miradi hiyo inakuwa bora na inayokidhi viwango.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Asajile Mwambambale amemshukuru Mheshimiwa Rrais wa awamu ya tano kwa namna ambavyo amekuwa akishirikiana na Wilaya ya Kilosa kwa kuipatia fedha mbalimbali katika miradi inayoendelea jambo ambalo limesaidia kwa kiasi kikubwa kusukuma mbele  guruduma la maendeleo ambapo fedha hizo zimekuwa zikitumika katika miradi ya sekta ya afya, miundombinu ya umwagiliaji na miradi mingineyo.

Pamoja na hayo Mwambambale amesema Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa imefanikiwa kutekeleza agizo la Mheshimiwa Rais wakati alipotembelea wilaya ya Kilosa Machi 13 mwaka huu na kuagizwa kujengwa jengo la upasuaji katika kituo cha afya Magubike agizo ambalo limetekelezwa ambapo kwasasa jengo hilo limekamilika na kujengwa kwa  fedha za mapato ya ndani na kugharimu kiasi cha shilingi milioni 103 ambazo zimetumika lengo ikiwa ni kudhibiti matumizi na kuokoa fedha za Serikali ambapo wilaya imekuwa ikifanya hivyo katika miradi mingine inayoendelea  ikiwemo ujenzi wa wodi mbili za wanawake na waume katika kituo cha afya Mikumi wodi ambazo kwa kiasi kikubwa ziko katika hatua za mwisho.

Akibainisha baadhi ya miradi mbalimbali ambayo imefanyika na inayoendelea kupitia mapato ya ndani Mwambambale amesema miradi hiyo ni ujenzi wa wodi mbili za kituo cha afya Mikumi, jengo la upasuaji kituo cha afya Magubike, ujenzi wa kituo cha afya Mvumi, ujenzi wa madarasa shule ya msingi Msowero huku akisema kuwa Halmashauri imejipanga kuongeza zaidi matumizi katika miradi ya maendeleo kwa kufikia 60% huku matumizi ya kawaida ikiwa 40% huku akisisitiza kuwa shauku ya Halmashauri kuwa na miradi ambayo thamani yake  inaonekana kwa macho zaidi.


Aidha katika ziara hiyo Mwenyekiti wa kamati ya huduma za jamii Mh Abdullatif Kaid amepongeza Halmashauri na Serikali kiujumla kwa juhudi mbalimbali ambazo zimekuwa zikionekana katika kuleta maendeleo kwa wananchi ambapo wananchi kiujumla katika kata zenye miradi ya afya wameshukuru kwa ujenzi wa majengo ambalimbali ya kutolea huduma unaoendelea kwani kwa kiasi kikubwa utawaondolea adha kwenda kutafuta huduma za afya maeneo ya mbali  jambo linalowagharimu muda, matumizi ya fedha nyingi na kutembea umbali mrefu.


Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa