• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

NMB YATOA MADAWATI 70 SHULE YA MSINGI MSOWERO

Posted on: June 7th, 2019

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya Mipango, Takwimu na Ufatiliaji Francis Kaunda ameushukuru uongozi wa benki ya NMB kwa juhudi zake za dhati katika kuunga mkono shughuli za maendeleo katika sekta ya elimu kwa kukabidhi madawati 70 yenye thamani ya shilingi milioni tano katika shule ya Msingi Msowero.

Kaunda ametoa shukrani hizo Juni 07 mwaka huu wakati wa makabidhiano ya madawati hayo ambapo amesema kuwa halmashauri inaahidi kuyatunza madawati hayo lakini pia amezitaka shule mbalimbali kuendelea kujenga vyumba vya madarasa ili kuweza kukidhi mahitaji na kwamba Serikali ya awamu ya Tano na Halmashauri iko bega kwa bega katika ujenzi huo kwa kuhakikisha vyumba hivyo vinakamilika na wanafunzi kupata mazingira mazuri ya kujifunzia.

Kaunda amesisitiza ujenzi wa maboma kwani licha ya Serikali  kuweka nguvu yake katika ujenzi huo lakini pia amesema wapo wadau mbalimbali wa elimu wakiwemo NMB ambao wako tayari kuunga mkono juhudi zinazofanyika kwa kuhakikisha licha upatikanaji wa vyumba vya madarasa vilivyokamilika lakini pia upatikanaji wa madawati, meza, viti na mabati vinapatikana.

Naye Meneja Mahusiano Biashara ya Serikali kanda ya Mashariki Anneth Kwayu kwa kushirikiana na Meneja wa NMB tawi la Kilosa Assey Mfinanga wamesema NMB ni mdau wa maendeleo hivyo wanao wajibu wa kuchangia shughuli za maendeleo  na kwamba kwao kuchangia sekta ya elimu ni jambo la kipaumbele ikiwa ni sehemu ya kurejesha sehemu ya faida kwa jamii kwa kuhakikisha changamoto za jamii zinapatiwa ufumbuzi kwa kujenga afya bora na elimu bora kwa jamii ya kitanzania huku wakisistiza Ofisi ya Mkurugenzi kutosita kuwashirikisha katika shughuli za maendeleo hasa katika sekta ya afya na elimu.

Aidha Mkuu wa Idara ya Elimu Msingi Christina Hauli ametoa wito kwa wazazi katika shule mbalimbali za msingi hasa zinazotarajia kuwa na makambi kwa ajili ya wanafunzi wa darasa la saba ili kuwa na muda mzuri wa kujisomea kutoa ushirikiano wa kutosha kwa uongozi wa shule kwa kuhakikisha watoto wao wanakuwa katika mazingira mazuri ya kujisomea na kupata chakula cha kutosha kwa wanafunzi ili kuwa na chachu ya ufaulu na kuiletea sifa wilaya ya Kilosa kwa kuwa na kiwango kizuri cha ufaulu.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa