• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

ONGEZENI JUHUDI UJENZI KITUO CHA AFYA MIKUMI - NAIBU KATIBU MKUU CCM BARA

Posted on: January 15th, 2019

Naibu Katibu Mkuu CCM Bara ambaye pia ni mlezi wa mkoa wa Morogoro Mh Rodrick Mpogolo ametoa wito kwa uongozi wa Halmashauri kuongeza bidii katika ujenzi wa kituo cha afya Mikumi  ili huduma za afya zianze kwani eneo hilo ni eneo lenye wakazi wengi, hivyo linastahiki kuwa na kituo cha afya ambapo huduma za afya zitakapoanza zitakua na manufaa kwa wananchi.

Aidha Mpogolo ametoa rai kwa watumishi wa afya pamoja na watumishi wa umma kwa ujumla kutoa huduma stahiki zenye ufanisi kwa wananchi pasipo kuomba rushwa kwani ni jambo la faraja kwa wananchi kupata huduma za afya katika hali nzuri ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Mh Rais kwa kuwajali wananchi.

Sambamba na hayo ametoa pongezi kwa wananchi kwa namna walivyoshiriki katika ujenzi wa kituo hicho kwa kushiriki katika shughuli mbalimbali ikiwemo kuchimba msingi, kumwaga zege la msingi na jamvi, ujazaji vifusi kwa majengo yote manne ambapo kiujumla nguvu za wananchi zilizotumika zimegharimu shilingi 15,103,240.000.

Naye sambamba na hayo Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe S. Kebwe ameishukuru Serikali ya awamu ya Tano kwa ajili ya kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya maendeleo ya wananchi huku akisisitiza ujenzi katika vituo vya afya mkoa wa Morogoro kuendelea kufanyika usiku na mchana na kwamba upatikanaji wa dawa uko vizuri, huku Mbunge wa jimbo la Kilosa Mh. Mbarak Bawazir amesema kuwa kutokana na changamoto ya maji ataongeza nguvu kwa kuchimba kisima ili maji yaweze kupatikana muda wote kwani eneo hilo ni eneo linalohitaji huduma za maji muda wote na ya kutosha.

Akisoma taarifa yake kwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Mganga Mkuu wa Halmashauri Dkt. Halima Mangiri amesema kuwa katika kutekeleza azma ya kuboresha miundombinu ya kutolea huduma za afya Serikali imetoa shilingi milioni 400 kwa ajili ya kujenga/kukarabati majengo katika kituo cha afya Mikumi ambapo mradi huo umejumuisha jengo la upasuaji, wodi ya wazazi, maabara na jengo la wagonjwa wa nje na kwamba Halmashauri ianatarajia kusimamia mradi ukamilike kwa wakati sambamba na kuendelea kuhamamsisha na kuelimisha wananchi ushiriki wao katika miradi ya maendeleo.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa